Wednesday, December 5, 2007

TUSISUBIRI RAIS ATUANDIKIE BARUA ZA KUTUFUKUZA KAZI TUZISAINI!
*Wazembe wengi serikalini wanakingiwa vifua na vigogo
*Ni tatizo sugu kwa nchi za Dunia ya Tatu

DANIEL MBEGA
Dar es Salaam

MKURUGENZI Mtendaji wa TANESCO kajiuzulu! Hii ni taarifa ambayo bado ya moto kabisa miongoni mwa Watanzania baada ya mtendaji mkuu wa Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania, Dk. Idris Rashid, kuamua kuachia ngazi baada ya kutofautiana na wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa shirika hilo kuhusu uamuzi wake wa kutaka kuongeza tarifu za umeme kwa asilimia 40.

Uamuzi huo umepingwa kwa muda mrefu na wanaharakati wengi hasa ikizingatiwa kwamba gharama za sasa tu bado zinawapiga chenga wananchi wa kawaida wanaotumia nishati hiyo, ambao ni asilimia 10 tu kati ya Watanzania wote milioni 37, huku asilimia 8 kati yao ni wa mijini na asilimia 2 ni vijijini.

Wengi wamepinga uamuzi huo kwa sababu badala ya kuweka mikakati ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata nishati hiyo hasa katika kipindi hiki cha sayansi na teknolojia, Tanesco inataka kuwanyang’anya hata wale wachache wanaoitumia kwa sasa. Kwa maana hiyo wataendelea kujenga ukuta mrefu zaidi wa kuzuia wale wasio nayo kuendelea kuikosa milele.

Inawezekana Dk. Idris Rashid akawa amejiuzulu kutokana na kusakamwa kwa uamua wake huo, lakini wachunguzi wa mambo wanajaribu kutafakari kwamba, kujiuzulu kwake kumekuja wakati ‘mbaya’ hasa baada ya Kamati Teule ya Kuchunguza Mikataba ya Madini kuanza kuchunguza kashfa ya Richmond.

Baadhi ya watu wanahisi kwamba, kwa kuwa tayari kamati hiyo, chini ya Jaji Mark Bomani, imeshaanza kuchunguza mkataba wa Richmond na Tanesco unaodaiwa kuzingirwa na ufisadi mkubwa, huenda mtendaji huyo wa Tanesco akawa ameamua kutafuta mahali alipoangukia ili ang’atuke, kupanda kwa tarifu za umeme kukawa ni mahali muafaka kwake.

Japokuwa hakuwepo wakati mkataba huo ukisainiwa, ambao pia unasemekana ulikuwa na shinikizo kutoka kwa vigogo wa juu serikalini waliokiuka taratibu za zabuni za serikali, lakini ameona bora aondoke katika kipindi hiki cha kashfa ya kupanda kwa umeme, tatizo ambalo kwa hakika linaweza kuathiri hata uzalishaji na shughuli zote za maendeleo na uchumi.

Vyovyote iwavyo, kujiuzulu tayari amejiuzulu, na niseme tu ukweli kwamba, hata kabla ya kujiuzulu tayari nilikuwa nimepanga kuandika makala haya ili kuhoji uhalali wa viongozi wetu wa Tanzania, Kiafrika na hata wa nchi zinazoendelea, kuwa na tabia ya kung’ang’ania madaraka hata pale wanapokuwa wamekumbwa na kashfa nzito zinazohusu maslahi ya jamii na taifa kwa ujumla.

Tangu serikali ya Awamu ya Nne chini ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete iingie madarakani siku 701 zilizopita (Desemba 21, 2005), watendaji wake wengi, wakiwemo mawaziri na wakurugenzi, wamekumbwa na kashfa nyingi zisizo na idadi na daima wameendelea kuwa makaidi hata pale wanapoelezwa ukweli.

Zipo tuhuma ambazo wamezifanya wakati wa utawala uliopita, wakishirikiana kwa namna moja ama nyingine na watawala waliopita, lakini pia zipo ambazo zimefanyika katika kipindi cha awamu hii nab ado wahusika wameendelea kuziba masikio, huku wakubwa wao nao wakiwafumbia macho na kuleta tafsiri ya kulindana.

Inaelezwa kwamba kashfa ya Benki Kuu kuhusiana na malipo ya akaunti ya madeni ya nje (EPA) yanayowahusisha watu wengi kuchota mamilioni ya fedha ilikuwa inajulikana muda mrefu eti hata kabla ya vyombo vya habari na Wabunge kulivalia njuga. Kwamba madai hayo yalikwishatolewa ufafanuzi na eti kulikuwa na watu waliokuwa wakiyakuza.

Gavana wa BoT, Daudi Balali akagoma kujiuzulu japo ukweli unaonekana dhahiri kwamba kuna ufisadi na mazingira ya rushwa yaliyotanda kwenye chombo hicho kuhusiana pia na mikataba mbalimbali, ukiwemo wa ujenzi wa minara miwili ya makao makuu ya Benki Kuu.

Watu waliohusika na ununuzi wa ndege ya rais, ununuzi wa rada ya bei mbaya, ununuzi wa helikopta za kijeshi na magari ya jeshi, uuzaji wa viwanja vya serikali na rasilimali za umma kwa bei ya kutupa, wote wapo na wanafahamika, lakini pamoja na ufisadi wao kufichuliwa, bado wameendelea kukalia viti vya enzi wakisema hawaondoki hata iweje.

Suala la mikataba feki na ile iliyozingirwa na rushwa liko wazi. Watendaji wengi wa serikali katika awamu iliyopita wanajulikana kwa sababu walifanya hivyo huku wakiwa katika madaraka yao, lakini pamoja na kufahamika kwa tuhuma zao hakuna hatua ambayo mpaka sasa imechukuliwa.

Ukiwaachilia hao waliofanya ufisadi kipindi hicho, wapo wale ambao bado wangali madarakani, wakiwemo gavana wa Benki Kuu Daudi Balali, na waziri wa nishati na madini Nazir Karamagi, ambaye tuhuma za mikataba ‘mibovu’ ya madini ndizo zilizoleteleza kuundwa kwa kamati teule yenye wajumbe wengi akiwemo Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe (CHADEMA) ambaye alitoa hoja binafsi kuhusiana na mkataba wa uchimbaji wa madini katika mgodi wa Buzwagi.

Inavyoonekana ni kwamba, viongozi wengi wa nchi zinazoendelea, ikiwemo Tanzania, hawana desturi ya kung’atuka pindi mambo yanapokuwa yamekwenda kombo, hata pale ukweli unapowekwa bayana, kama ilivyo sasa kwa kashfa zinazowakabili Karamagi na Balali pamoja na watendaji wengi wa serikali.

Taratibu za ‘kulindana’ baina ya viongozi wa juu serikali, wa kati na wale wa chini, ndizo zilizoshika hatamu nchini Tanzania kiasi kwamba mtu anaona hawezi kuguswa hata kama ufisadi uliofanyika umeigharimu serikali na jamii kwa ujumla kiasi kikubwa sana cha fedha.

Nakumbuka mwaka 2001 wakati treni ilipoanguka nchini India waziri aliyekuwa akihusika na usafirishaji alilazimika kujiuzulu. Treni tu! Kwani yeye ndiye aliyelipindua? Lakini hiyo ndiyo gharama ya siasa, kwa sababu alijua kwamba tukio hilo limetokea chini ya uongozi wake na kama kulikuwa na uzembe wowote ungeweza kujulikana baadaye yeye akiwa pembeni kutoa nafasi ya uchunguzi.

Leo hii viongozi wengi wa Tanzania hawataki kuwajibika wakati hata nafsi zao zinawasuta bayana kwamba wamefanya uzembe. Lakini kutokana na kiburi walicho nacho, kilichopandikizwa kutoka juu mpaka chini kwa kutumia kanuni isiyojulikana ya ‘Wakubwa kulindana’, waheshimiwa hawa wamekuwa kama miungu-watu ambao daima wanaona hawawezi kunyooshewa hata kidole na awaye yote.

Ni jambo lililo dhahiri kwamba kuna matatizo katika nchi zetu, na viongozi wanapaswa kuwajibika mara matatizo yanapotokea. Tusisubiri ifikie mahali Rais akaandika barua ya kukufukuza kazi na kukuletea uisaini! Nadhani hiyo itakuwa aibu kubwa na fedheha isiyostahimilika.

Katika kipindi cha awamu ya tatu tulishuhudia mawaziri wanne na manaibu wao wawili wakijiuzulu kutokana na kashfa mbalimbali. Kwanza mwaka 1996 Waziri wa Fedha Profesa Simon Mbilinyi na naibu wake Kilontsi Mpologomyi walilazimika kujiuzulu baada ya kuibuka kwa kashfa ya misamaha ya kodi ya minofu ya samaki na mafuta kwa makampuni kadhaa.

Hoja iliyosababisha kung’atuka kwa mawaziri hao ilitolewa binafsi na Mbunge wa Ilala wa wakati ule, Idd Mohammed Simba, ambaye baadaye aliteuliwa kuwa mwenyekiti wa kamati teule iliyoundwa kuchunguza kashfa hiyo.

Baadaye aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Juma Ngasongwa, naye alilazimika kujiuzulu kutoa nafasi ya uchunguzi baada ya kutajwa katika ripoti ya Tume ya Kero ya Rushwa ya Jaji Joseph Warioba kwamba alikuwa amehusika kwa namna moja ama nyingine na suala la minofu ya samaki.

Miaka miwili baadaye aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Dk. Hassy Kitine, naye alilazimika kujiuzulu. Mkurugenzi huyo wa zamani wa Idara ya Usalama wa Taifa alijiuzulu baada ya kuibuka kwa kashfa ya kumtibu mkewe nje ya nchi kwa kutumia mamilioni ya fedha za serikali kinyume cha taratibu. Hapo ndipo unapoweza kujiuliza, msimamizi wa utawala bora anavunja kanuni kinyemela kama hivyo.

Oktoba 7, 1998 aliyekuwa naibu waziri wa fedha Bi Monica Mbega, naye akaandika barua kuomba kujiuzulu kwa maelezo kwamba anakwenda kusoma. Rais Benjamin Mkapa alimkubalia, ingawa wachunguzi wa masuala ya kisiasa walihusisha kujiuzulu kwake na kashfa ya kuwapeleka ‘ndugu zake’ Ureno (ambao walizamia huko huko) katika mkutano wa dunia wa vijana, wakati huo akiwa naibu waziri wa kazi na maendeleo ya vijana.

Ndipo hatimaye Novemba 4, 2001 Idd Simba akatangaza kujiuzulu uwaziri wa viwanda na biashara kufuatia kashfa ya sukari, baada ya tume ya Jaji Bernard Michael Luanda kubainisha kwamba kulikuwa na ukiukwaji wa taratibu katika utoaji wa vibali kwa makampuni yaliyokuwa yanaagiza sukari nje ya nchi baada ya nchi kukumbwa na hali mbaya ya uhaba wa sukari.

Hoja iliyoleteleza Simba kujiuzulu ilitolewa na Mbunge wa Kwela, Chrisant Majiyatanga Mzindakaya ‘Mzee wa Mabomu’, lakini pamoja na serikali ‘kuiteka’ hoja hiyo na kuunda tume yake badala ya Tume ya Bunge, ukweli ulianikwa hadharani kwamba makampuni mengi kati ya yale yaliyokuwa yameruhusiwa yalikuwa yameingizwa kinyume cha taratibu.

Lakini nakumbuka siku ambayo Mzindakaya alitoa hoja binafsi Agosti 10, 2001 pale Dodoma, almanusura Idd Simba atangaze kujiuzulu siku hiyo hiyo kwa sauti ya upole, yenye mashaka pale aliposema; “…Kupitia Bunge lako tukufu,” akasita kwa sekunde chache “…napenda kuwasalimu wananchi wa Ilala na wananchi wote kwa ujumla na niseme sijalidanganya Bunge na sijihusishi na vitendo vyovyote vya rushwa.”

Licha ya tuhuma za sukari, pia Idd Simba alikuwa anakabiliwa na tuhuma za kukiuka maagizo ya Baraza la Mawaziri na Ikulu katika kubinafsisha Kampuni ya Taifa ya Wakala wa Meli (NASACO) ambayo ilikuwa inajiendesha kwa faida.

Haya ni baadhi tu ya mambo yaliyokuwa yamejitokeza katika awamu ya tatu, ingawa yalikuwepo mengi yaliyofichika ambayo sasa yamefichuliwa na wahusika wapo, lakini kwa vile wengine walishirikiana na viongozi wa juu serikalini, wanaona kwamba hawawezi kufanywa kitu chochote kwa kuwa walioshirikiana nao hawaguswi na sheria kikatiba!

Yawezekana hizi zikawa ni ndoto za wengi wanaoingia madarakani, madaraka ambayo walio wengi wanayanunua kwa bei kubwa sana na wanapopewa nyadhifa wanataka kwanza kuziba mapengo ya gharama walizotumia wakati huo.

Hata hivyo, hatudhani kama huu ni ustaarabu kwa mtu kuharibu mali ya umma kwa kisingizio kwamba unakula na wakubwa. Umechaguliwa kwa ajili ya kuwatumikia wananchi ambao hasa ndio waajiri wako na unapokiuka maadili ya uongozi unakuwa umewatendea dhambi kubwa wale waliokupa dhamana ya kuwaongoza.

Hivi kweli waheshimiwa hawa wanataka turejee enzi zile za awamu ya kwanza ambapo tulishuhudia mawaziri na viongozi kadhaa wa serikali wakitangazwa kustaafishwa kwa manufaa ya umma? Ni kwa nini wasiwe waungwana kwa kuamua kuwajibika, wakajiuzulu na kukaa kando kama alivyofanya Alhaj Ali Hassan Mwinyi enzi zile alipokuwa Waziri wa Mambo ya Ndani kabla hajawa Rais wa Jamhuri ya Muungano?

Tunaamini kwamba kwa mtu muungwana, kujiuzulu ni uamuzi wa busara mara linapotokea tatizo zito kama haya tunayoyaona, wala si dhambi au aibu. Tumeshuhudia hata katika mataifa yaliyoendelea jinsi mawaziri na viongozi mbalimbali wanapoamua kujiuzulu wanapokabiliwa na kashfa, kwa nini sisi tnaoendelea tunakuwa wagumu?

Utawala bora unahitaji busara na hekima ya kutosha, kinyume chake tunakuwa na serikali iliyojaa miungu-watu wanaopenda kujiamulia mambo yao wenyewe, ambao hawako tayari kukosolewa. Tunahitaji kubadilika kama kweli tunataka kujenga taifa lenye nidhamu. Ada ya mja kunena, muungwana ni vitendo!

Mwisho.

No comments:

JUST ANOTHER THOUGHT

JUST ANOTHER THOUGHT

A person asked God, “What surprises you most about mankind?”

And God answered,
“That they loose their Health to make money and they loose their money to restore their Health.

That by thinking anxiously about the future, they forget the present, such that they live neither for the present nor the future.

That they live as if they will never die and they die as if they had never lived.….”

BECAUSE I'M A MAN...

Because I’m a man, when one of our appliances stops working I will insist on taking it apart, despite evidence that this will just cost me twice as much once the repair person gets here and has to put it back together.

Because I’m a man, I don’t think we’re all that lost, and no, I don’t think we should stop and ask someone. Why would you listen to a complete stranger I mean, how the hell could he know where we’re going?

Because I’m a man, there is no need to ask me what I’m thinking about. The answer is always either sex or football, though I have to make up something else when you ask, so don’t.

Because I’m a man, I do not want to visit your mother, come visit us, or talk to her when she calls, or think about her any more than I have to. Whatever you got her for mother’s day is okay, I don’t need to see it. And don’t forget to pick up something for my mommy, too!

Because I’m a man, I am capable of announcing, “one more beer and I really have to go”, and mean it every single time I say it, even when it gets to the point that the one bar closes and my buddies and I have to go hunt down another. I will find it increasingly hilarious to have my pals call you to tell you I’ll be home soon, and no, I don’t understand why you threw all my clothes into the front yard. Like, what’s the connection?

Because I’m a man, you don’t have to ask me if I liked the movie. Chances are, if you’re crying at the end of it, I didn’t.

Because I’m a man, yes, I have to turn up the radio when Bruce Springsteen or The Doors comes on, and then, yes, I have to tell you every single time about how Bruce had his picture on the cover of Time and Newsweek the same day, or how Jim Morrison is buried in Paris and everyone visits his grave. Please do not behave as if you do not find this fascinating.

Because I’m a man, I think what you’re wearing is fine. I thought what you were wearing five minutes ago was fine, too. Either pair of shoes is fine. With the belt or without it looks fine. Your hair is fine. You look fine. Can we just go now?

Because I’m a man and this is, after all, the 90’s, I will share equally in the housework. You just do the laundry, the cooking, the gardening, the cleaning, and the dishes. I’ll do the rest.

A SIMPLE GUIDE TO LIFE

1. Follow your dream! Unless it’s the one where you’re at work in your underwear during a fire drill.

2. Always take time to stop and smell the roses and sooner or later, you’ll inhale a bee.

3. Do not walk behind me, for I may not lead. Do not walk ahead of me, for I may not follow. Do not walk beside me, either. Just leave me alone.

4. If you don’t like my driving, don’t call anyone. Just take another road. That’s why the highway department made so many of them.

5. If a motorist cuts you off, just turn the other cheek. Nothing gets the message across like a good mooning.

6. When I’m feeling down, I like to whistle. It makes the neighbor’s dog run to the end of his chain and gag himself.

7. It’s always darkest before dawn. So if you’re going to steal the neighbor’s newspaper, that’s the time to do it.

8. A handy telephone tip: Keep a small chalkboard near the phone. That way, when a salesman calls, you can hold the receiver up to it and run your fingernails across it until he hangs up.

9. Each day I try to enjoy something from each of the four groups: the bonbon group, that salty-snack group, the caffeine group and the “What ever-it-is-the-tinfoil-in-the-back-of-the-fridge”.

10. Into every life some rain must fall. Unusually when your car windows are down.

11. Just remember: You gotta break some eggs to make a real mess on the neighbor’s car!

12. When you find yourself getting irritated with someone, try to remember that all men are brothers and just give them a noogie.

13. This morning I woke up to the unmistakable scent of pigs in a blanket. That’s the price you pay for letting the relatives stay over.

14. It’s a small world. So you gotta use your elbows a lot.

15. Keep your nose to the grindstone and your shoulder to the wheel. It’s a lot cheaper than plastic surgery.

16. This land is your land. This land is my land. So stay in your land.

17. Love is like a roller coaster: When it’s good you don’t want to get off, and when it isn’t, you can’t wait to throw up.

DEDICATION TO YOUNG PEOPLE

Youth is a time of hope. Also of uncertainty. But for a person who is young and healthy, uncertainty just means a challenge. It is important to be positive. First of all about yourself. But also about your family and your people. As a unique person and each human being are unique, you have enormous potential. Because you have so much potential, people may sometimes feel negatively challenged by that potential and try to undermine it.

You have to fight for your right to make your place in society. To do that you have to use all the chances given you now to be a positive element in whatever situation you find yourself in, in future. So, it may be necessary to be a ‘rebel in reverse’ as it were. That takes real courage, to set your goal and stick to it. You choose your crowd. You exercise your right to choose.
Don’t lose your freedom for the sake of anyone. Real freedom, freedom to choose the right thing, the best for you.

Always bear a few things in mind while exercising your right to choose.

* Never take a decision when you are in a fit of anger or depression.
* Never take a decision when you are emotionally high.
* Why should fads or the decision of the group tie you down?
* What are you?
* What do you want tomorrow to be for you?

No matter how strong the group decision may be, you must think and make your decision. Many times it is necessary to consult before taking a decision. Go to someone whose life you admire, not necessarily the person you like most, but the person who is whole, who is one person, wherever she or he is and whatever she or he does.

* Remember that there is always tomorrow, and tomorrow is hope. Very few things are ‘written in stone’. Most of the mistakes we make can be rectified. They can be corrected. Problems have a solution, and each new day is a new start, a new chance, a New Hope. Indeed the youth are our hope you are our future.

Also remember that your parents love you unconditionally, you have their support and want the best in life for you ¨

COSTA VICTOR NAMPOKA

Mguu ulivyokatisha ndoto za kucheza soka Ulaya

DANIEL MBEGA
Dar es Salaam

NI majira ya saa 5.20 hivi asubuhi, niko hapa Ukonga-Banana nikiwania kupanda daladala la kwenda kwenye kitongoji cha Kitunda-Kibeberu, moja ya vitongoji vinavyokua kwa kasi hapa jijini Dar es Salaam.
Sijui ni umbali gani kutoka hapa, hivyo namuuliza dereva ambaye nimeketi naye pembeni yake. Ananiambia ni mwendo kama wa dakika 15 tu hivi. Nashusha pumzi kwa kujua kwamba kumbe si mbali sana kama nilivyofikiria.
Nawasili kwenye kitongoji cha Kibeberu, ambako ndiko magari yanakogeuzia, na bila kupoteza muda nampigia simu mwenyeji wangu kwamba tayari nimeshafika. Namhurumia huko aliko kama ataamua kuja kunipokea, lakini nafarijika anaponiambia kwamba nimuulize mtu yeyote hapo kituoni atanileta.
Watoto wawili wanajitolea kunipeleka nyumbani kwa mwenyeji wangu, ambaye namkuta akiwa kajilaza kwenye kochi akizungumza na rafiki zake wawili waliomtembelea. Anapenda kuketi vizuri, lakini hali haimruhusu.
“Poleni jamani kwa safari ndefu!” ndivyo anavyoanza kusema huyu mwenyeji wangu, ambaye si mwingine zaidi ya mlinzi mahiri wa timu ya soka ya Taifa, Taifa Stars, pamoja na klabu ya Simba, Costa Victor Nampoka ‘Nyumba’. Anajaribu kuuweka vyema mguu wake wa kulia ambao bado umefungwa bandeji gumu (POP) baada ya kuvunjia mazoezini takribani mwezi mmoja na nusu uliopita.
“Hakuna shaka, Dar es Salaam ni moja na hakuna sehemu unayoweza kusema ni mbali,” namjibu kumpa matumaini.
“Hapana! Pamoja na ukweli kwamba mkoa kazini, lakini naamini uamua kufunga safari mpaka kuja kuniona ni jambo kubwa sana. Mngeweza hata kuniuliza maendeleo yangu kwa njia ya simu. Sina budi kushukuru kwa kuja kunijulia hali,” anasema.
Mara anaingia dada mmoja mweupe hivi ambaye anaketi pamoja na Costa kwenye kochi moja. Costa mwenyewe anamtambulisha kwamba ndiye mkewe, Dina, ambaye wamebahatika kuzaa naye watoto wawili; Victor Costa mwenye miaka miwili na Rio Costa mwenye mwaka 1.5. Anatukaribisha.
Anapoondoka namwambia ni jambo la kawaida kuwatembelea wagonjwa, na katika suala lake yeye ni mmoja wa watu waliotoa mchango mkubwa katika timu ya taifa ya soka ambayo sasa iko katika nafasi nzuri ya kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika mwakani ikiwa tu itashinda mechi yake ya mwisho.
“Nashukuru kusikia hivyo, lakini sura zinazokuja hapa daima ni zile nilizozizowea, yaani marafiki zangu na wachezaji wenzangu wa klabu ya Simba, labda na viongozi wa Simba,” anasema kwa huzuni.
“Una maana kwamba viongozi wa timu ya taifa na hata TFF huwa hawakutembelei?” nauliza.
Anasema tangu alipoumia siku tatu kabla ya Taifa Stars kupambana na Zambia katika mechi ya kirafiki na kupelekwa Muhimbili na daktari wa timu Shecky Mngazija, hajatembelewa wala kujuliwa hali hata kwa simu na kiongozi yeyote yule wa chombo hicho cha juu cha soka nchini.
Anaongeza kwamba, ni wachezaji wenzake wa Simba ndio baadhi yao huwa wanawasiliana naye pamoja na viongozi na marafiki wa klabu ambao wameonekana kumjali vya kutosha kiasi cha kutuma gari kila siku katika mechi zote ambazo Simba ilicheza kwenye hatua ya Sita Bora ya Ligi ya Mpito hadi fainali.
“Kwa kweli viongozi wa klabu yangu wananijali sana na sina budi kuwashukuru,” anasema. Kama vile amekumbuka kitu, anasema anamshukuru pia mtu mmoja wa Benki ya NMB anayeitwa Kajura (Imani Kajura ambaye ni Meneja Masoko).
“Huyu jamaa baada ya kutoa zawadi za shilingi 500,000 kwa kila mchezaji kutokana na timu ya Taifa kushinda kule Burkina Faso, alinipigia simu kuniambia nilitakiwa kwenda kusaini fomu za akaunti. Nikamwambia sina hata pesa ya nauli na kwa jinsi ninavyoumwa nisingeweza kupanda daladala, lakini akaniambia nichukue teksi nay eye angelipa. Namshukuru sana,” anasema.
Hata hivyo, amewaasa wachezaji wengine; wa klabu na hata timu ya taifa, kwamba pindi watakapoumia na kushindwa kujuliwa hali na viongozi wao wasife moyo bali hiyo iwe changamoto kwao kufanya vizuri watakaporejea uwanjani.
“Binafsi sina kinyongo na yeyote. Naomba Mungu nipone nirejee uwanjani, ikibidi niliwakilishe taifa langu, kwa sababu natambua kwamba timu ya Taifa ni ya Watanzania wote wala si ya mtu mmoja. Naamini Watanzania milioni kadhaa wako pamoja na mimi na hata walipojua kwamba nimeumia walinitumia meseji za pole zaidi ya 3,000, hata sijui walikoipata namba yangu,” anasema.

Kuvunjika mguu
Costa anasema kwamba walikuwa kwenye mazoezi kama kawaida kwenye uwanja wa Karume, akauzuia mpira bila kumkwatua ama kukwatuliwa, kisha akaserereka.
“Ghafla nikasikia maumivu makali sana, ikabidi wajaribu kuniganga pale, lakini yalipozidi wakanikimbiza Muhimbili. Huko nikaambiwa kwamba nimevunjika mfupa mdogo wa mguu wa kulia. Sikuwa na jinsi, wakanifunga hogo (bandeji gumu – POP) na kusema kwamba nirudi baada ya wiki sita,” anasema kwa majonzi.
Anasema kwamba, baada ya kutolewa kwa bandeji hilo ndipo atakapojua kama atakuwa nje ya uwanja kwa muda gani, kwani mpaka sasa hajaanza hata kuukanyangia mguu huo.
Akasema kuvunjika mguu kumemnyima nafasi ya kuliwakilisha taifa, na zaidi kumechelewesha kutimia kwa ndoto zake kwani pengine hivi sasa angeweza kuwa Afrika Kusini kujaribu kucheza soka ya kulipwa akiwa njiani kwenda cheza Ulaya.
“Kuna wakala mmoja ambaye kwa muda mrefu sasa amekuwa akinufuatilia, yuko Afrika Kusini, na alikwenda Burkina Faso kunitazama, lakini mimi sikuwepo. Ilikuwa niende Afrika Kusini kufanya majaribio na naamini ningewea kufanikiwa,” anasema mchezaji huyo.
Anasema kwamba, alikuwa na matumaini ya kufuzu kwa sababu soka ya Afrika Kusini haina tofauti na ya huku, tena hakuwa mgeni baada ya kucheza kwa muda nchini humo miaka mitatu iliyopita.
“Wanachotuzidi kule ni promosheni, televisheni zinajitahidi sana kuonyesha mpira hata wa daraja la tatu, na hiyo inamsaidia mchezaji kutazama na kuona wapi alipokosea ili kujirekebisha, ama afanye nini kuongeza jitihada,” anasema.
Anaongeza kwamba alishindwa kuendelea kucheza huko kwa sababu klabu aliyokuwa akiichezea wakati ule ya Marlasburg (Tembas) iliyokuwa daraja la kwanza mwaka 2005 ikiwa chini ya kocha wa zamani wa Simba Trott Moloto, iliinunua klabu moja iliyokuwa ligi kuu. Ikabidi wachezaji wa timu hizo wachekechwe, na majungu ndipo yakaibuka ambapo Moloto, ambaye ndiye aliyemfanyia mpango wa kwenda huko, akamgeuka. Ikabidi afungashe virago kurejea.
Hata hivyo, anasema kwamba ndoto zake bado hazijafutika, kwani anaamini anaweza kucheza Ulaya bila matatizo yoyote, na zaidi anasema angependa siku moja avae ‘uzi’ wa Manchester United akicheza pembeni ya Rio Ferdnand ambaye uchezaji wake unamvutia kiasi cha kumwitia mwanawe mdogo jina hilo kutokana na kumhusudu.
Akizungumzia nafasi ya Taifa Stars kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika mwakani, Costa (25) ambaye ni mtoto wa nne katika familia ya watoto watano wa mzee Victor Nampoka – wawili wanawake na watatu wanaume, anasema kwamba nafasi ipo, lakini mechi ya mwisho dhidi ya Msumbiji ni ngumu sana.
“Ile mechi ni kama fainali na inabidi maandalizi ya nguvu yafanyike pengine kuliko mechi zote zilizotangulia. Msumbiji ni wazuri sana kuliko hata Burkina Faso, na ina nafasi ya kufuzu ikiwa itashinda na Senegal wakafungwa, hivyo Watanzania tusibweteke bali tujiandae vizuri,” anasema huku akisikitika kwamba anaweza kuikosa mechi hiyo pia ikiwa ataambiwa apumzike.
Akizungumzia kuhusu maendeleo ya soka, mlinzi huyo anasema kwamba hakuna kitakachoinua zaidi ya soka la vijana, na kuongeza kwamba mashindano ya Copa Coca Cola yawe chachu wa klabu na wadau mbalimbali kuanza kuibua vipaji.
“Kule Brazil tulikokwenda kuna taasisi ya soka ya watoto wadogo. Watoto wanatoka nchi mbalimbali kwenda kufundishwa mpira, na wazazi wao wanalipia wastani wa dola 1,500 kwa mwezi ili watoto wao wajue mpira. Tusione wenzetu wamepiga hatua tukadhani kwamba ni miujiza, wamewekeza.
“Watanzania wanapaswa kuunga mkono juhudi za maendeleo ya soka ya vijana, kuanzia kwa wazazi, ambao wanapaswa kuwapa ‘sapoti’ watoto wao ikiwa ni pamoja na kuwapatia vifaa vya michezo na nauli ya kwenda mazoezini,” anaongeza.
Costa aliyemaliza elimu ya msingi mwaka 1994 Kinondoni Hananasif, jijini Dar es Salaam na kuungana na maelfu ya watoto ambao hawakufanikiwa kuchaguliwa kujiunga na sekondari, amewashauri wachezaji kuachana na anasa na kwamba wawe na malengo kama kweli wanataka kupiga hatua katika mchezo huo.
“Sijafanikiwa sana, lakini niseme ukweli kwamba nimejiepusha na mambo mengi. Sivuti sigara wala bangi, halafu niliacha kitambo kunywa pombe, tena basi nilikuwa nikinywa bia mbili ama tatu tu, lakini sasa sitaki kabisa nahitaji kukazana kwenye mpira ambao pekee ndio mwokozi wangu katika maisha,” anamalizia.

Wasifu:
Jina: Costa Victor Nampoka
Kuzaliwa: Oktoba 11, 1982, Dar es Salaam.
Umri: 25

Klabu za awali:
Five Star Kinondoni, Mkunguni FC Ilala, Eleven FC Buguruni, Saddam FC na International FC za Kinondoni.
Taifa Jang’ombe – Zanzibar (1998 – 1999)
Forodha Zanzibar (2000 – 2001)
Mtibwa Sugar (2002)
Simba (2003 – 2004)
Marlsburg – Afrika Kusini (2005)
Simba (2006 – mpaka sasa).