Wednesday, December 5, 2007

BIASHARA ILIVYOFUTA UTAKATIFU WA IKULU!
*Nyerere hakujua kama aliowatetea ni wajasiriamali wa kubwa

DANIEL MBEGA
Dar es Salaam

WAKATI wa mchakato wa kumtafuta mgombea wa urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu wa kwanza wa vyama vingi Tanzania mwaka 1995 tulishuhudia wanaccm wengi wakijitokeza kuwania nafasi hiyo adhimu kwa tiketi ya chama hicho.

Miongoni mwao, ambao nilihudhuria hata mikutano yao ya kutangaza azma zao za kuwania nafasi hiyo walikuwemo mawaziri wakuu watatu wastaafu; Jaji Joseph Sinde Warioba, John Samuel Melecela na Cleopa David Msuya.

Wanaccm wengine walikuwa Katibu Mkuu wa chama hicho wakati huo Horace Kolimba, Jaji Mark Bomani, Jakaya Mrisho Kikwete, Edward Ngoyayi Lowassa na mgombea ‘asiyefahamika’ wakati huo Benjamin William Mkapa.

Kuibuka kwa wagombea wengi kiasi hicho ndani ya CCM kuliwafanya Watanzania waamini kwamba ile demokrasia iliyokuwa imefichwa kwa miaka mingi na utawala wa chama kimoja ilikuwa imeibuka na kukomaa. Wananchi sasa waliamini walikuwa na nafasi ya kumchagua mgombea yeyote waliyedhani anafaa badala ya kupewa karatasi ya kura yenye picha ya mtu mmoja na kivuli huku wakilazimika kupiga kura za ‘NDIYO’ au ‘HAPANA’.

Lakini pia kuibuka kwa wanaccm wengi kiasi hicho kulimpagawisha sana mtu mmoja; Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ambaye aliamini kwamba hiyo haikuwa demokrasia tena bali chama kilikuwa kimevamiwa na kwamba kilikuwa na viongozi ‘wabaya’, ambao dhahiri aliwaona walikuwa na nguvu na wangeweza kupitishwa na chama kushika madaraka ya nchi.

Pengine kilichomshtua zaidi ni kule kuona Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, John Malecela, ambaye hakuwa amejitokeza mapema kama wenzake, akiibuka ghafla na kupata wadhamini 250,000 waliotakiwa huku akiungwa mkono na kundi kubwa la vijana na baadhi ya wazee.

Akiwa tayari ametajwa mapema kwamba alikuwa anakusudia kumpigia debe mgombea wa upinzani, Mwalimu Nyerere akawaonya wale wabaya ndani ya chama waliokuwa na nguvu kwamba; “Wasipotupatia mgombea mzuri, hawatutawali… Kama hawatuwekei mgombea mzuri, kwa nini watutawale?”

Nyerere aliona kabisa kwamba chama kilikuwa kimevamiwa na watu wenye fedha, ambao walikuwa tayari kumsimika ‘mtu wao’ kwa kutumia fedha hizo ambazo Mwalimu Nyerere aliwahi kuziita ‘fedha za bangi’, akimaanisha kwamba zilikuwa fedha chafu ambazo hata upatikanaji wake ulikuwa wa njia zisizo halali ndiyo maana walikuwa tayari kuzitumiza watakavyo ili kulinda ‘maslahi’ yao.

Lakini pia inaonekana Nyerere alishtushwa zaidi na kuibuka na vijana wawili ambao baadaye walikuja kupachikwa jina la ‘Boys II Men’; Jakaya Kikwete na Edward Lowassa, ambao wakati wa kurejesha fomu za kuwania kuteuliwa kugomea urais kule Dodoma walikodi ndege ya binafsi. Ni huko ambako tunaambiwa Mwalimu aliwahi kuwauliza wagombea, akiwemo Lowassa, ni wapi walikozipata fedha walizokuwa nazo.

Lakini majina yale yalipochujwa na Kamati Kuu ya CCM katika mchakato wa kwanza na kubaki matatu – Msuya, Mkapa na Kikwete – Nyerere alisikika akisema kwamba; “Rais bora angetoka CCM,” na akamtaja Ben Mkapa kwamba ndiye aliyekuwa bora zaidi kati ya wale watatu. Huyu mwingine wa mwisho, Kikwete, aliambiwa kwamba kura zake hazikutosha na kwamba asubiri mpaka kipindi kingine.

Mwalimu akamnadi Ben kila pembe ya nchi huku akisema “Mgombea wa CCM anauzika.” Aliweka matumaini makubwa kwamba mgombea huyo mara atakaposhinda na kutwaa madaraka angeweza kufuata falsafa zake na kujenga taifa lililo imara katika misingi ya haki, usawa, uadilifu na uwajibikaji.

Lakini kabla kampeni rasmi za kitaifa hazijaanza, wanaccm wengi wakatoka na kujiunga na vyama vya upinzani huku baadhi yao, akiwemo Augustine Lyatonga Mrema, wakionekana kuwa na mvuto mkubwa sana kwa wananchi.

Mwalimu akasimama kidete kuwaponda wagombea hao huku akitamka bayana; “I cant let this country to the dogs (Siwezi kuwaachia mbwa nchi hii),” kauli ambayo wapinzani waliifananisha na kashfa kwao kufananishwa na mbwa ingawa kihalisia Nyerere hakuwa amemaanisha hivyo.

Nyerere akashika hatamu za kampeni kwa nguvu zote akimpamba na kumsifu ‘mteule’ wake – Mkapa. Kwa kuwa tayari alikuwa amewaponda viongozi wengine wa serikali na chama kama Malecela na kolimba kwenye kitabu chake cha ‘Uongozi wetu na hatma ya Tanzania’, aliweza kuzibadili fikra za wananchi wengi ili wamshabikie mgombea wake.

Akawaponda wagombea wengine wa vyama vya upinzani waliokuwa kwenye mchakato huo akisema; “Mnakimbilia Ikulu, Ikulu kuna biashara gani pale? Mnataka kwenda kufanya nini Ikulu? Ikulu ni mahali patakatifu, si mahali pa mchezo mchezo pale. Ni mahali pa kuheshimika!”

Ndiyo. Kauli hizi na nyinginezo alizozitoa Mwalimu ziliwagusa wengi na wakaamini kwamba chaguo lake – Mkapa – lilikuwa sahihi mno. Mkapa, ambaye awali wengi walimkejeli kwamba hajulikani kimataifa tofauti na akina Warioba, Malecela na Msuya, sasa akawa maarufu hata kabla ya kuingia Ikulu.

Hizi ndizo falsafa za Mwalimu Nyerere ambazo zilisaidia Tanganyika ikapata uhuru wake kwa kutumia nguvu ya hoja. Alimudu kuiongoza Tanzania kwa miaka 24 si kwa sababu ya usomi wake na kuzungumza kwake, bali karama ya uongozi ilikuwa ndani yake.

Hata hivyo, kitu pekee ambacho hakukijua ni kwamba, miaka michache baadaye wale aliodhani wangefuata falsafa yake wakawa wamekengeuka na kuamua kuitia najisi Ikulu, sehemu takatifu ambayo Nyerere alipigania kuhakikisha hakiingii kilicho ‘kichafu’.

Yaliyofanyika pale Ikulu, ambayo kama leo hii Nyerere angekuwa hai, hakika angeweza kulia machozi, tena ya damu, kwa kuona kwamba kumbe juhudi zake za kuwapiga vijembe wengine waliotaka kupaendea mahali pale pa juu palipoinuka zikuwa bure kabisa hasa baada ya wale alioamini kwamba wangepaenzi kuamua kuyafanya yale yale aliyokuwa akiyakataza!

Leo hii Watanzania wengi walikuwa wanaombea walau Mwenyezi Mungu angempa uhai zaidi Mwalimu Nyerere wa kuweza “kumuona rais wa awamu ya nne” kama alivyokuwa amesema mwenyewe siku ile ya ‘birthday’ yake ya miaka 75 mwaka 1997, hakika angeweza kushuhudia ufisadi mkubwa ambao ulikuwa unafanywa na wale ambao aliamini wangeyafanya ‘mapenzi ya baba’.

Kilichotokea ni kama ule mfano wa wana wawili, ambapo mkubwa alitumwa na babaye aende shambani, lakini akakataa kwamba hatakwenda, lakini baadaye akabadili mawazo na kwenda. Mdogo akatumwa aende, akasema atakwenda, lakini baadaye hakwenda! Ni nani aliyeyafanya mapenzi ya baba kama si yule wa kwanza?

Mwalimu alikuwa amefanya kazi na wakongwe wengi ambao walijitokeza katika mchakato ule wa mwaka 1995, lakini kwa kuwa huko nyuma walikuwa wamekosea na kuona kwamba hawafai, akaamua kumpigia chapuo ‘mdogo wao’ Mkapa, ambaye ‘alimuahidi’ kwamba angekwenda kutekeleza yale aliyotumwa. Lakini kwa bahati mbaya zaidi, wale wakongwe ambao walikuwa wamekosea huko nyuma walikuwa wamejirekebisha na kuwajibika iwapasavyo, na yule ambaye aliaminiwa kwamba ndiye angeweza kutekeleza mapenzi ya Mwalimu, akafanya ndivyo sivyo.

Mwalimu Nyerere alifariki Oktoba 14, 1999, lakini kwa kudhihirisha kwamba mwanafunzi wake Mkapa alikuwa amemsaliti, tayari alikuwa ameanzisha kampuni ya kibiashara akiwa Ikulu, miezi mitatu na siku 22 kabla Mwalimu hajaaga dunia, yaani Juni 22, 1999 wakati Mkapa na mkewe mama Anna, wakati huo wakiwa madarakani, walipoanzisha kampuni ya ANBEM Limited. Kampuni hiyo ni kifupishi cha majina yao, yaani Anna na Ben Mkapa.

Wakati hayo yakitokea, tayari serikali ilikuwa imeshachafuliwa na kashfa kadhaa za mawaziri wa serikali ya awamu ya tatu, ambapo kwanza Waziri wa Fedha Profesa Simon Mbilinyi na naibu wake Kilontsi Mpologomyi walikuwa wamejiuzulu kutokana na kashfa ya misamaha ya kodi kwa mafuta na minofu ya samaki, Waziri wa Maliasili na Utalii Dk. Juma Ngasongwa alikuwa amejiuzulu baada ya kutajwa katika Tume ya Kero ya Rushwa ya Jaji Joseph Warioba kuhusiana na minofu ya samaki, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora) Dk. Hassy Kitine alikuwa amejiuzulu kwa kashfa ya kumtibia mkewe nje ya nchi kwa mamilioni ya fedha za serikali kinyume cha utaratibu, na naibu waziri wizara ya fedha Monica Mbega alijiuzulu kwa madai ya kwenda kusoma, ingawa wachunguzi wa masuala ya siasa walikuwa wamehusisha kujiuzulu kwake na kashfa ya kuwapeleka ndugu zake kwenye mkutano wa dunia wa vijana jijini Lisbon, Ureno, ambako inasemekana walizamia moja kwa moja.

Tangu hapo viongozi waliokuwa Ikulu ya Tanzania wkaendelea kufanya biashara, tena wakitumia ofisi za serikali, ambapo tunaambiwa kwamba Julai 2002 kampuni ya ANBEM ilichukua mkopo wa Dola za Marekani 500,000 (takribani milioni 620/-) kutoka benki ya NBC, ambayo ilibinafsishwa kwa kuingia ubia na Benki ya ABSA ya Afrika Kusini pamoja na Mwalimu Nyerere, enzi ya uhai wake, kupinga kwa nguvu zote kwamba chombo hicho kisibinafsishwe. Mwezi Desemba ANBEM ikachukua mkopo mwingine wa milioni 250/- kutoka benki ya CRDB.

Miaka miwili baadaye tukashuhudia kuanzishwa ka kampuni nyingine ya Tanpower Resources (ilisajiliwa Desemba 29, 2004), ambayo taarifa za wachunguzi zinabainisha kwamba inamilikiwa na Rais mstaafu Benjamin Mkapa (wakati huo akiwa bado madarakani) na mkewe kupitia kampuni yao ya ANBEM Limited, motto wao Nicholas kupitia kampuni yao na mkewe Foster Mbuna iliyoanzishwa mwaka huo huo iitwayo Fosnik Enterprises Limited.

Wengine wanaotajwa kumiliki hisa za Tanpower Resources Company Limited ni pamoja na Waziri wa Nishati na Madini (wakati huo) Daniel Ndhira Yona na mwanawe Danny kupitia kampuni yao ya DEVCONSULT Limited (Yona ana hisa 90% kwenye kampuni hiyo na mwanawe ana 10%), baba mkwe wa Nicholas Mkapa, Joseph Mbuna, kupitia kampuni yake ya Choice Industries Limited, na kampuni ya Universal Technologies Limited inayomilikiwa kwa pamoja na Evans Mapundi na Wilfred Malekia.

Kampuni ya Tanpower Resources ambayo Machi 2006 iliingia mkataba na Tanesco wa kuzalisha umeme wa Megawatts 200 katika mgodi wa makaa yam awe wa Kiwira, mkoani Mbeya wenye thamani ya Dola za Marekani milioni 271.8 (takribani bilioni 340/-) mbali ya kuanzishwa na viongozi ambao walikuwa bado wako Ikulu, lakini pia inamilikiwa na familia, au kwa kifupi ni ya ukoo!

Lakini si hao tu, ziko kashfa nyingi zinazoendelea ndani ya serikali yetu ya sasa na ile iliyopita. Kwa mfano; inakumbukwa jinsi jinsi Benki Kuu ilivyoingia mkenge kwa kulipa mabilioni ya fedha kufidia deni la kampuni iliyoibuka ghafla na kufa ya Meremeta Gold Mine, ambayo ilirithiwa na kampuni ya Tangold.

Tunaambiwa kwamba kampuni ya Tangold, ambayo ilisajiliwa Aprili 2005 mjini Port Louis, Mauritius, ilikuwa inamilikiwa na viongozi wakubwa serikalini wakiwemo Gavana wa Benki Kuu Daudi Ballali, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Gray Mgonja, Mwanasheria Mkuu wa wa Serikali (wakati huo enzi ya Mkapa) Andrew John Chenge, Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Patrick Rutabanzibwa na Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Mifugo Vincent Mrisho.

Ballali na Mgonja bado wanaendelea kuzishikilia nyadhifa zao mpaka sasa, wakati Rutabanzibwa ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Mrisho ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu.

Hakika haya ni matumizi mabaya ya madaraka kwa sababu ni kinyume kabisa na kanuni za maadili ya utawala bora na utumishi wa umma ibara ya 12 hadi ya 14, na kama Nyerere angalikuwa hai leo akaona namna wapendwa wake, wale aliowateua ‘wanywee kikombe cha bwana wao’, wanavyoyatumia vibaya madaraka yao, kwa kuwapora wananchi mkate wao.

Tuwafananishe na nani viongozi wa zama hizi basi? Tuwafananishe na Mfalme Daudi aliyemtwaa Baarsheba kuwa mkewe kutoka kwa Uria, ambaye aliamua kumuua ili amtwae moja kwa moja? Au tuwafananishe na Mfalme Nebukadneza wa Babeli aliyejitukuza na kujiona kama yuko karibu na Mungu kabla ya kufukuziwa porini kula umande kwa miaka mitatu na nusu kabla ya kutambua kwamba utawala wa wanadamu unawekwa na Mungu?!

Watawala hawa wameonyesha kumkosoa Mwalimu Nyerere kwa vitendo, kwamba kama alidhani Ikulu hakuna biashara, basi wao wameweza kuifanya, tena wakiwa hawana hofu wala woga wa aina yoyote, huku wakisimama majukwaani kusisitiza utawala bora.

Tunataka tuwe na watawala bora, lakini viongozi wa aina hii ambao wanaonekana kuinajisi Ikulu na ofisi za umma hakika wanapandikiza mbegu mbaya kwa vijana wetu, ambao nao wanaendelea kuiga mle mle walimopitia wazee wao na kuzidi kulifanya taifa hili kuwa la watu wasiokuwa makini, ambao ufisadi kwao ni kama kitu kilichohalalishwa.

Laiti kama Nyerere angefufuka leo na kuona jinsi alivyosalitiwa, hakika angeifuta kauli yake kwamba wale aliodhani ‘mbwa’ walikuwa bora zaidi kuliko hawa!

Mwisho.

No comments:

JUST ANOTHER THOUGHT

JUST ANOTHER THOUGHT

A person asked God, “What surprises you most about mankind?”

And God answered,
“That they loose their Health to make money and they loose their money to restore their Health.

That by thinking anxiously about the future, they forget the present, such that they live neither for the present nor the future.

That they live as if they will never die and they die as if they had never lived.….”

BECAUSE I'M A MAN...

Because I’m a man, when one of our appliances stops working I will insist on taking it apart, despite evidence that this will just cost me twice as much once the repair person gets here and has to put it back together.

Because I’m a man, I don’t think we’re all that lost, and no, I don’t think we should stop and ask someone. Why would you listen to a complete stranger I mean, how the hell could he know where we’re going?

Because I’m a man, there is no need to ask me what I’m thinking about. The answer is always either sex or football, though I have to make up something else when you ask, so don’t.

Because I’m a man, I do not want to visit your mother, come visit us, or talk to her when she calls, or think about her any more than I have to. Whatever you got her for mother’s day is okay, I don’t need to see it. And don’t forget to pick up something for my mommy, too!

Because I’m a man, I am capable of announcing, “one more beer and I really have to go”, and mean it every single time I say it, even when it gets to the point that the one bar closes and my buddies and I have to go hunt down another. I will find it increasingly hilarious to have my pals call you to tell you I’ll be home soon, and no, I don’t understand why you threw all my clothes into the front yard. Like, what’s the connection?

Because I’m a man, you don’t have to ask me if I liked the movie. Chances are, if you’re crying at the end of it, I didn’t.

Because I’m a man, yes, I have to turn up the radio when Bruce Springsteen or The Doors comes on, and then, yes, I have to tell you every single time about how Bruce had his picture on the cover of Time and Newsweek the same day, or how Jim Morrison is buried in Paris and everyone visits his grave. Please do not behave as if you do not find this fascinating.

Because I’m a man, I think what you’re wearing is fine. I thought what you were wearing five minutes ago was fine, too. Either pair of shoes is fine. With the belt or without it looks fine. Your hair is fine. You look fine. Can we just go now?

Because I’m a man and this is, after all, the 90’s, I will share equally in the housework. You just do the laundry, the cooking, the gardening, the cleaning, and the dishes. I’ll do the rest.

A SIMPLE GUIDE TO LIFE

1. Follow your dream! Unless it’s the one where you’re at work in your underwear during a fire drill.

2. Always take time to stop and smell the roses and sooner or later, you’ll inhale a bee.

3. Do not walk behind me, for I may not lead. Do not walk ahead of me, for I may not follow. Do not walk beside me, either. Just leave me alone.

4. If you don’t like my driving, don’t call anyone. Just take another road. That’s why the highway department made so many of them.

5. If a motorist cuts you off, just turn the other cheek. Nothing gets the message across like a good mooning.

6. When I’m feeling down, I like to whistle. It makes the neighbor’s dog run to the end of his chain and gag himself.

7. It’s always darkest before dawn. So if you’re going to steal the neighbor’s newspaper, that’s the time to do it.

8. A handy telephone tip: Keep a small chalkboard near the phone. That way, when a salesman calls, you can hold the receiver up to it and run your fingernails across it until he hangs up.

9. Each day I try to enjoy something from each of the four groups: the bonbon group, that salty-snack group, the caffeine group and the “What ever-it-is-the-tinfoil-in-the-back-of-the-fridge”.

10. Into every life some rain must fall. Unusually when your car windows are down.

11. Just remember: You gotta break some eggs to make a real mess on the neighbor’s car!

12. When you find yourself getting irritated with someone, try to remember that all men are brothers and just give them a noogie.

13. This morning I woke up to the unmistakable scent of pigs in a blanket. That’s the price you pay for letting the relatives stay over.

14. It’s a small world. So you gotta use your elbows a lot.

15. Keep your nose to the grindstone and your shoulder to the wheel. It’s a lot cheaper than plastic surgery.

16. This land is your land. This land is my land. So stay in your land.

17. Love is like a roller coaster: When it’s good you don’t want to get off, and when it isn’t, you can’t wait to throw up.

DEDICATION TO YOUNG PEOPLE

Youth is a time of hope. Also of uncertainty. But for a person who is young and healthy, uncertainty just means a challenge. It is important to be positive. First of all about yourself. But also about your family and your people. As a unique person and each human being are unique, you have enormous potential. Because you have so much potential, people may sometimes feel negatively challenged by that potential and try to undermine it.

You have to fight for your right to make your place in society. To do that you have to use all the chances given you now to be a positive element in whatever situation you find yourself in, in future. So, it may be necessary to be a ‘rebel in reverse’ as it were. That takes real courage, to set your goal and stick to it. You choose your crowd. You exercise your right to choose.
Don’t lose your freedom for the sake of anyone. Real freedom, freedom to choose the right thing, the best for you.

Always bear a few things in mind while exercising your right to choose.

* Never take a decision when you are in a fit of anger or depression.
* Never take a decision when you are emotionally high.
* Why should fads or the decision of the group tie you down?
* What are you?
* What do you want tomorrow to be for you?

No matter how strong the group decision may be, you must think and make your decision. Many times it is necessary to consult before taking a decision. Go to someone whose life you admire, not necessarily the person you like most, but the person who is whole, who is one person, wherever she or he is and whatever she or he does.

* Remember that there is always tomorrow, and tomorrow is hope. Very few things are ‘written in stone’. Most of the mistakes we make can be rectified. They can be corrected. Problems have a solution, and each new day is a new start, a new chance, a New Hope. Indeed the youth are our hope you are our future.

Also remember that your parents love you unconditionally, you have their support and want the best in life for you ¨

COSTA VICTOR NAMPOKA

Mguu ulivyokatisha ndoto za kucheza soka Ulaya

DANIEL MBEGA
Dar es Salaam

NI majira ya saa 5.20 hivi asubuhi, niko hapa Ukonga-Banana nikiwania kupanda daladala la kwenda kwenye kitongoji cha Kitunda-Kibeberu, moja ya vitongoji vinavyokua kwa kasi hapa jijini Dar es Salaam.
Sijui ni umbali gani kutoka hapa, hivyo namuuliza dereva ambaye nimeketi naye pembeni yake. Ananiambia ni mwendo kama wa dakika 15 tu hivi. Nashusha pumzi kwa kujua kwamba kumbe si mbali sana kama nilivyofikiria.
Nawasili kwenye kitongoji cha Kibeberu, ambako ndiko magari yanakogeuzia, na bila kupoteza muda nampigia simu mwenyeji wangu kwamba tayari nimeshafika. Namhurumia huko aliko kama ataamua kuja kunipokea, lakini nafarijika anaponiambia kwamba nimuulize mtu yeyote hapo kituoni atanileta.
Watoto wawili wanajitolea kunipeleka nyumbani kwa mwenyeji wangu, ambaye namkuta akiwa kajilaza kwenye kochi akizungumza na rafiki zake wawili waliomtembelea. Anapenda kuketi vizuri, lakini hali haimruhusu.
“Poleni jamani kwa safari ndefu!” ndivyo anavyoanza kusema huyu mwenyeji wangu, ambaye si mwingine zaidi ya mlinzi mahiri wa timu ya soka ya Taifa, Taifa Stars, pamoja na klabu ya Simba, Costa Victor Nampoka ‘Nyumba’. Anajaribu kuuweka vyema mguu wake wa kulia ambao bado umefungwa bandeji gumu (POP) baada ya kuvunjia mazoezini takribani mwezi mmoja na nusu uliopita.
“Hakuna shaka, Dar es Salaam ni moja na hakuna sehemu unayoweza kusema ni mbali,” namjibu kumpa matumaini.
“Hapana! Pamoja na ukweli kwamba mkoa kazini, lakini naamini uamua kufunga safari mpaka kuja kuniona ni jambo kubwa sana. Mngeweza hata kuniuliza maendeleo yangu kwa njia ya simu. Sina budi kushukuru kwa kuja kunijulia hali,” anasema.
Mara anaingia dada mmoja mweupe hivi ambaye anaketi pamoja na Costa kwenye kochi moja. Costa mwenyewe anamtambulisha kwamba ndiye mkewe, Dina, ambaye wamebahatika kuzaa naye watoto wawili; Victor Costa mwenye miaka miwili na Rio Costa mwenye mwaka 1.5. Anatukaribisha.
Anapoondoka namwambia ni jambo la kawaida kuwatembelea wagonjwa, na katika suala lake yeye ni mmoja wa watu waliotoa mchango mkubwa katika timu ya taifa ya soka ambayo sasa iko katika nafasi nzuri ya kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika mwakani ikiwa tu itashinda mechi yake ya mwisho.
“Nashukuru kusikia hivyo, lakini sura zinazokuja hapa daima ni zile nilizozizowea, yaani marafiki zangu na wachezaji wenzangu wa klabu ya Simba, labda na viongozi wa Simba,” anasema kwa huzuni.
“Una maana kwamba viongozi wa timu ya taifa na hata TFF huwa hawakutembelei?” nauliza.
Anasema tangu alipoumia siku tatu kabla ya Taifa Stars kupambana na Zambia katika mechi ya kirafiki na kupelekwa Muhimbili na daktari wa timu Shecky Mngazija, hajatembelewa wala kujuliwa hali hata kwa simu na kiongozi yeyote yule wa chombo hicho cha juu cha soka nchini.
Anaongeza kwamba, ni wachezaji wenzake wa Simba ndio baadhi yao huwa wanawasiliana naye pamoja na viongozi na marafiki wa klabu ambao wameonekana kumjali vya kutosha kiasi cha kutuma gari kila siku katika mechi zote ambazo Simba ilicheza kwenye hatua ya Sita Bora ya Ligi ya Mpito hadi fainali.
“Kwa kweli viongozi wa klabu yangu wananijali sana na sina budi kuwashukuru,” anasema. Kama vile amekumbuka kitu, anasema anamshukuru pia mtu mmoja wa Benki ya NMB anayeitwa Kajura (Imani Kajura ambaye ni Meneja Masoko).
“Huyu jamaa baada ya kutoa zawadi za shilingi 500,000 kwa kila mchezaji kutokana na timu ya Taifa kushinda kule Burkina Faso, alinipigia simu kuniambia nilitakiwa kwenda kusaini fomu za akaunti. Nikamwambia sina hata pesa ya nauli na kwa jinsi ninavyoumwa nisingeweza kupanda daladala, lakini akaniambia nichukue teksi nay eye angelipa. Namshukuru sana,” anasema.
Hata hivyo, amewaasa wachezaji wengine; wa klabu na hata timu ya taifa, kwamba pindi watakapoumia na kushindwa kujuliwa hali na viongozi wao wasife moyo bali hiyo iwe changamoto kwao kufanya vizuri watakaporejea uwanjani.
“Binafsi sina kinyongo na yeyote. Naomba Mungu nipone nirejee uwanjani, ikibidi niliwakilishe taifa langu, kwa sababu natambua kwamba timu ya Taifa ni ya Watanzania wote wala si ya mtu mmoja. Naamini Watanzania milioni kadhaa wako pamoja na mimi na hata walipojua kwamba nimeumia walinitumia meseji za pole zaidi ya 3,000, hata sijui walikoipata namba yangu,” anasema.

Kuvunjika mguu
Costa anasema kwamba walikuwa kwenye mazoezi kama kawaida kwenye uwanja wa Karume, akauzuia mpira bila kumkwatua ama kukwatuliwa, kisha akaserereka.
“Ghafla nikasikia maumivu makali sana, ikabidi wajaribu kuniganga pale, lakini yalipozidi wakanikimbiza Muhimbili. Huko nikaambiwa kwamba nimevunjika mfupa mdogo wa mguu wa kulia. Sikuwa na jinsi, wakanifunga hogo (bandeji gumu – POP) na kusema kwamba nirudi baada ya wiki sita,” anasema kwa majonzi.
Anasema kwamba, baada ya kutolewa kwa bandeji hilo ndipo atakapojua kama atakuwa nje ya uwanja kwa muda gani, kwani mpaka sasa hajaanza hata kuukanyangia mguu huo.
Akasema kuvunjika mguu kumemnyima nafasi ya kuliwakilisha taifa, na zaidi kumechelewesha kutimia kwa ndoto zake kwani pengine hivi sasa angeweza kuwa Afrika Kusini kujaribu kucheza soka ya kulipwa akiwa njiani kwenda cheza Ulaya.
“Kuna wakala mmoja ambaye kwa muda mrefu sasa amekuwa akinufuatilia, yuko Afrika Kusini, na alikwenda Burkina Faso kunitazama, lakini mimi sikuwepo. Ilikuwa niende Afrika Kusini kufanya majaribio na naamini ningewea kufanikiwa,” anasema mchezaji huyo.
Anasema kwamba, alikuwa na matumaini ya kufuzu kwa sababu soka ya Afrika Kusini haina tofauti na ya huku, tena hakuwa mgeni baada ya kucheza kwa muda nchini humo miaka mitatu iliyopita.
“Wanachotuzidi kule ni promosheni, televisheni zinajitahidi sana kuonyesha mpira hata wa daraja la tatu, na hiyo inamsaidia mchezaji kutazama na kuona wapi alipokosea ili kujirekebisha, ama afanye nini kuongeza jitihada,” anasema.
Anaongeza kwamba alishindwa kuendelea kucheza huko kwa sababu klabu aliyokuwa akiichezea wakati ule ya Marlasburg (Tembas) iliyokuwa daraja la kwanza mwaka 2005 ikiwa chini ya kocha wa zamani wa Simba Trott Moloto, iliinunua klabu moja iliyokuwa ligi kuu. Ikabidi wachezaji wa timu hizo wachekechwe, na majungu ndipo yakaibuka ambapo Moloto, ambaye ndiye aliyemfanyia mpango wa kwenda huko, akamgeuka. Ikabidi afungashe virago kurejea.
Hata hivyo, anasema kwamba ndoto zake bado hazijafutika, kwani anaamini anaweza kucheza Ulaya bila matatizo yoyote, na zaidi anasema angependa siku moja avae ‘uzi’ wa Manchester United akicheza pembeni ya Rio Ferdnand ambaye uchezaji wake unamvutia kiasi cha kumwitia mwanawe mdogo jina hilo kutokana na kumhusudu.
Akizungumzia nafasi ya Taifa Stars kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika mwakani, Costa (25) ambaye ni mtoto wa nne katika familia ya watoto watano wa mzee Victor Nampoka – wawili wanawake na watatu wanaume, anasema kwamba nafasi ipo, lakini mechi ya mwisho dhidi ya Msumbiji ni ngumu sana.
“Ile mechi ni kama fainali na inabidi maandalizi ya nguvu yafanyike pengine kuliko mechi zote zilizotangulia. Msumbiji ni wazuri sana kuliko hata Burkina Faso, na ina nafasi ya kufuzu ikiwa itashinda na Senegal wakafungwa, hivyo Watanzania tusibweteke bali tujiandae vizuri,” anasema huku akisikitika kwamba anaweza kuikosa mechi hiyo pia ikiwa ataambiwa apumzike.
Akizungumzia kuhusu maendeleo ya soka, mlinzi huyo anasema kwamba hakuna kitakachoinua zaidi ya soka la vijana, na kuongeza kwamba mashindano ya Copa Coca Cola yawe chachu wa klabu na wadau mbalimbali kuanza kuibua vipaji.
“Kule Brazil tulikokwenda kuna taasisi ya soka ya watoto wadogo. Watoto wanatoka nchi mbalimbali kwenda kufundishwa mpira, na wazazi wao wanalipia wastani wa dola 1,500 kwa mwezi ili watoto wao wajue mpira. Tusione wenzetu wamepiga hatua tukadhani kwamba ni miujiza, wamewekeza.
“Watanzania wanapaswa kuunga mkono juhudi za maendeleo ya soka ya vijana, kuanzia kwa wazazi, ambao wanapaswa kuwapa ‘sapoti’ watoto wao ikiwa ni pamoja na kuwapatia vifaa vya michezo na nauli ya kwenda mazoezini,” anaongeza.
Costa aliyemaliza elimu ya msingi mwaka 1994 Kinondoni Hananasif, jijini Dar es Salaam na kuungana na maelfu ya watoto ambao hawakufanikiwa kuchaguliwa kujiunga na sekondari, amewashauri wachezaji kuachana na anasa na kwamba wawe na malengo kama kweli wanataka kupiga hatua katika mchezo huo.
“Sijafanikiwa sana, lakini niseme ukweli kwamba nimejiepusha na mambo mengi. Sivuti sigara wala bangi, halafu niliacha kitambo kunywa pombe, tena basi nilikuwa nikinywa bia mbili ama tatu tu, lakini sasa sitaki kabisa nahitaji kukazana kwenye mpira ambao pekee ndio mwokozi wangu katika maisha,” anamalizia.

Wasifu:
Jina: Costa Victor Nampoka
Kuzaliwa: Oktoba 11, 1982, Dar es Salaam.
Umri: 25

Klabu za awali:
Five Star Kinondoni, Mkunguni FC Ilala, Eleven FC Buguruni, Saddam FC na International FC za Kinondoni.
Taifa Jang’ombe – Zanzibar (1998 – 1999)
Forodha Zanzibar (2000 – 2001)
Mtibwa Sugar (2002)
Simba (2003 – 2004)
Marlsburg – Afrika Kusini (2005)
Simba (2006 – mpaka sasa).