Friday, May 14, 2010

Kilimo hai ni mkombozi pekee wa mkulima wa Tanzania
*Serikali yatakiwa kuhamasisha mboji badala ya chumvichumvi
*Bidhaa za kilimo hai zinaongoza soko duniani, hazina madhara

Na Mwandishi Wetu,
Dar es Salaam

Kilimo ndio msingi wa maisha ya binadamu, na kwa Mtanzania, tunaambiwa daima kwamba kilimo ndio uti wa mgongo wa uchumi, kikiwa kinachangia asilimia kubwa ya pato la taifa, na pia kilimo ndiye mwajiri wa takriban asilimia 80 ya Watanzania.

Kama viongozi wetu walivyopata kutueleza, ili tuweze kupata maendeleo, ni lazima kuwepo na vitu vitatu: Ardhi, Uongozi Bora na Siasa Safi. Tayari vitu hivi vipo kwa sababu taifa letu linaendeshwa kwa misingi ya demokrasia, na ardhi ipo ya kutosha.

Hata hivyo, ni lazima kutambua kwamba, ardhi ama udongo ndiyo rasilimali mama ulimwenguni. Madini ya thamani yanapatikana ardhini, miti ya mbao inapatikana ardhini pamoja na mimea ya kila aina, bila kusahau kwamba viumbe hai wengine, binadamu na hayawani wa mwituni, nao pia wanaitegemea ardhi kwa ajili ya ustawi wao, kwani udongo huu unatumika kuzalisha kitu chochote ambacho kinahitajika kwa matumizi ya binadamu na wanyama.

Tumeirithi ardhi kutoka kwa vizazi vilivyotangulia ikiwa na ubora wa asili, lakini kutokana na matumizi ya muda mrefu, ardhi hii huzeeka na kushindwa kutoa mazao bora juu yake, hivyo kumfanya binadamu kutafuta namna nyingine ya kuifanya ardhi hiyo itoe mazao bora.

Katika sehemu kubwa ya nchi yetu, ardhi imekuwa chanzo cha migogoro ya mara kwa mara kutokana na matumizi yake, ambapo jamii za wakulima na wafugaji zimekuwa zikigombana – na hata wakati mwingine kusababisha maafa – kila moja ikisema inastahili kutumia ardhi hii.

Hii ni kwa sababu mkulima, baada ya kuona ardhi yake imechoka huamua kutafuta maeneo mengine yaliyo bora na kuanza kuyatumia. Wakati mwingine hulazimika kufyeka misitu ili kupata mashamba mapya, hali ambayo siyo tu inaharibu mazingira, lakini pia inaweza kututia umaskini wa milele kwa sababu ardhi iliyoachwa awali huwa haitafutiwi njia muafaka ya kuifanya irejee kwenye ubora wake.

Katika baadhi ya maeneo, wakulima wengine hutafuta mbolea, hasa za chumvi chumvi, na kuzitumia katika ardhi ile inayoonekana kuzeeka. Lakini matatizo mengi huibuka kutokana na matumizi ya mbolea pamoja na madawa ya kemikali kwenye kilimo. Hii ni kwa sababu mbolea hizi zina kemikali na yale madawa ya kuua wadudu yana madhara yake kwani yana sumu isiyoonekana. Hii sumu tunakula au tunakunywa na ndizo zinazoleta madhara kwa binadamu na udongo.

Aidha, mazao yatokanayo na kilimo cha mbolea hizi za kemikali yanaleta athari kubwa zisizoonekana kwa binadamu na hata wanyama. Lakini jambo la kuzingatia kwa sasa, kila mtu anatakiwa kuvuta kumbukumbu zake kulingana na umri alioishi na kuangalia yafuatayo: Hali ya udongo enzi zile na sasa ikoje? Kiwango cha maradhi wakati ule na sasa kikoje? Uwezo wa udongo kuzalisha mazao umepungua au unazidi mwaka hadi mwaka?

Wengi wetu tumegundua kwamba mbolea za chumvichumvi zimechakaza udongo na hivyo kufanya uzalishaji upungue. Hata mazao yatokanayo na matumizi ya mbolea hizo yamekosa ubora wa asili unaotakiwa. Hii inatia shaka kama umaskini wa mkulima utakwisha ikiwa hatabadili aina ya pembejeo kuokoa ardhi yake isizidi kuchakaa, na wakati huo huo kupunguza sumu isiyoonekana kwenye udongo na vyanzo vya maji.

Katika mataifa mengi ya ulimwengu wa kwanza, mbolea za chumvi chumvi zinatumika kupandia na kukuzia miti, hasa ya mbao. Vile vile inatumika kutengenezea mazingira kwa maeneo ambayo hayatumiki kuzalisha mazao ya chakula cha binadamu. Wao wamekuwa wakipiga sana vita vyakula vilivyolimwa kwa kutumia mbolea za chumvi chumvi, na ndiyo maana hivi sasa katika soko la dunia, bidhaa zilizozalishwa kwa kutumia mbolea hizi za chumvi chumvi zimekuwa zikiuzwa kwa bei ya chini kuliko zile zinazolimwa kwa kutumia kilimo hai. Sasa tujiulize, kwa nini sisi tunaendelea kutumia mbolea hizi zinazoua udongo wetu na kuweka sumu? Hivi hakuna mbolea nyingine mbadala? Jibu ni kwamba, mbolea mbadala zipo.

Mbolea mbadala ni zile zinazotokana na uozo wa asili. Uozo wa asili unaotokana na majani mbalimbali, samadi ya mifugo asili; mabaki ya nafaka au mazao mbalimbali (kama maganda ya karanga, mabua ya mahindi, n.k.).

Mbolea hizi zinaweza kupatikana au kutengenezwa katika mazao tunayolima, kwenye mazingira tunayoishi. Mbolea hizi zinasaidia kurudisha udongo katika hali ya rutuba na asili yake na gharama za mbolea hizi ni nafuu kabisa na zinadumu ardhini kwa muda mrefu.

Jambo la kuzingatia ni kwamba, udongo ni mali pekee yenye thamani kubwa ambayo tumepewa na Mwenyezi Mungu. Hivi sasa kuna migogoro mingi vijijini kutokana na watu kukimbilia mashamba mapya kwa ajili ya kutafuta rutuba baada ya mashamba yao ya zamani kufa kutokana na matumizi ya mbolea zenye kemikali.

Ni ukweli usiopingika kwamba, mbolea za chumvi chumvi zikiisha muda wake hugeuka sumu na baadaye mkulima analazimika kutumia gharama kubwa kuweka mbolea za mboji ili kurudisha udongo katika hali nzuri. Sumu hii isiyoonekana inaharibu udongo, vyanzo vya maji na hata mwili wako mwenyewe.

Mkulima anahitaji kupata mazao bora na ya kutosha ili yamsaidie kwa chakula, na ziada inayopatikana auze kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya familia, lengo ambalo linaonekana kuwa gumu kufikiwa katika nyakati za sasa ambapo pembejeo za kilimo zimekuwa ghali na zaidi matumizi ya mbolea za kemikali yanazidi kuua ardhi, hivyo kupunguza uzalishaji wenyewe.

Aidha, hata mazao yatokanayo na kilimo cha mbolea za kemikali nayo hayana bei kubwa katika soko la dunia ikilinganishwa na mazao yatokanayo na kilimo hai, ambacho kwa sasa ndicho kinachohamasishwa ulimwenguni kwa sababu kinatumia viuatilifu asilia ambavyo siyo tu vinaongeza tija ya mazao, lakini pia ni rafiki wa mazingira, kama ilivyo kwa mbolea ya Erth Food inayoonekana kutelekezwa kwa sasa.

Kwa mfano, katika mwaka 2003/2004 wastani wa bei za mazao ya kilimo hai ilikuwa takriban asilimia 20 hadi 50 juu ya bei za mazao yasiyo ya kilimo hai katika Soko la Jumuiya ya Ulaya na Marekani. Kwa mwaka 2005/2006 kahawa iliyozalishwa kwa kilimo hai (organic coffee) iliuzwa kwa Dola za Kimarekani (USD) 65.7 kwa kilo 50 ikilinganishwa na USD 50.0 kwa kilo 50 za kahawa iliyozalishwa kwa kutumia kemikali za kilimo (agro-chemicals). Aidha, vanilla iliyouzwa nchi za Jumuiya ya Ulaya ilipata premium ya asilimia 20 hadi 300.

Kilimo hai au organic farming ni aina ya kilimo kinachozingatia matumizi endelevu ya rasilimali za uzalishaji wa mazao ya kilimo na mifugo. Kilimo hicho kinatumia mbolea na madawa yasiyotengenezwa viwandani na kinazingatia utunzaji wa mazingira kwa ajili ya manufaa kwa jamii, kiuchumi na kiafya.

Ili bidhaa zikubalike katika Soko la Kimataifa kuwa zimezalishwa kwa kutumia mbinu za kilimo hai, zinapaswa kwanza kupitishwa na Taasisi zinazosimamia ubora wa bidhaa hizo. Taasisi hizo ni International Federation of Organic Agriculture Movement (IFOAM) na Shirika la Ubora wa Viwango vya Vyakula la Umoja wa Mataifa (Codeaux Alimentarius Commission). Soko la mazao ya kilimo hai hutegemea walaji wa mazao hayo ambao wapo tayari kulipa bei kubwa kwa mazao ambayo yamezalishwa bila ya kutumia viatilifu na mbolea za viwandani.
Kilimo hai nchini kilianza kupata umaarufu katika miaka ya 1990 baada ya Serikali kuruhusu Taasisi kadhaa zisizo za Kiserikali (NGO) zikiwemo EGAJ, INADESTZ, PELUM, Meatu Cotton Projects, Babati LAMP na nyinginezo zilizojitokeza kueneza elimu na teknolojia za kilimo hai.

Aidha, Serikali kwa kutambua umuhimu wa kilimo hai na nia ya kuwasaidia wakulima kuendeleza kilimo hicho imeweka vipengele muhimu kwenye sera yake ya kilimo ikiwa ni pamoja na kuruhusu Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kusimamia biashara na bidhaa zake ambapo mwaka 2005 iliruhusu kuundwa kwa Tanzania Organic Agriculture Movement (TOAM) yenye lengo la kuwaunganisha wadau wa kilimo hai na kuwajengea uwezo.

Kutokana na juhudi hizo hivi sasa kilimo hai kinalimwa katika Mikoa ya Kilimanjaro, Tanga, Kigoma, Iringa, Pwani, Kagera, Mbeya, Morogoro, Shinyanga na Arusha. Mazao yanayozalishwa kwa njia ya mkataba ni pamoja na kahawa, chai, korosho, cocoa na pamba. Mazao mengine ni matunda na viungo hususan mananasi, tangawizi, tumeric, vanilla, pilipili na vitunguu. Sehemu kubwa ya bidhaa wanazozalisha zinauzwa moja kwa moja katika Soko la Jumuiya ya Ulaya na kiasi kidogo katika Soko la Marekani.

Hata hivyo, masharti yanayoambatana na kilimo hai yanakuwa magumu kwa baadhi ya wakulima na hivyo wakulima wengi kushindwa kuzalisha mazao hayo pamoja na kuwa yana bei kubwa. Wizara yangu itaendelea kushirikiana kwa karibu na Taasisi zinazoendeleza kilimo hai nchini ili kuhakikisha kwamba ubora wa mazao yanayozalishwa ni wa juu kulingana na viwango vya Kimataifa.
Utafiti wa kina unafanywa na Mashirika ya Nchi za Afrika Mashariki ambayo ni (Kenya Organic Agricultural Network (KOAN), National Organic Agricultural Movement of Uganda (NGAMU) na Tanzania Organic Agricultural Movement (TOAM) ili kuboresha uzalishaji na fursa za biashara ya bidhaa za kilimo hai katika nchi za Afrika Mashariki. Matokeo yatatolewa baada ya utafiti kukamilika.
Kilimo hai ni muhimu sana nchini Tanzania na mkombozi wa mkulima kwa kuwa kitamfanya kudumu mahali pamoja kwa muda mrefu na kuweza kujipanga vyema namna ya kujikwamua kimaisha. Pia kilimo hai kitainusuru nchi isigeuke jangwa kutokana na watu wanaokimbilia kufyeka misitu kwa minajiri ya kutafuta ardhi yenye rutuba, na zaidi kitasaidia kupunguza migogoro baina ya wakulima na wafugaji ambayo inatokea sasa.

Mikakati ya kuhamaisha kilimo hai ni elimu ya uhamasishaji ambayo inatakiwa ianzie ngazi ya chini, kwa mkulima mmoja mmoja, kwa vikundi tukitumia viongozi wa vijiji, kata, wilaya, mikoa na taifa ili kila mtu afahamu faida zake kwa ukamilifu.

Uwepo wa pembejeo za mboji nchini utamkwe kwa wananchi na serikali yenyewe. Hii itasaidia wakulima waelewe haraka na itasaidia kuharakisha watu wanaotaka kuweka miradi ya kutengeneza pembejeo hizo hapa nchini wapate mwelekeo mzuri.

Pembejeo za mboji pia zinapaswa kutambuliwa na kuingizwa kwenye ruzuku kama pembejeo zingine ili mkulima apate unafuu na serikali haipaswi kupendelea zaidi mbolea za kemikali.

Taasisi ya TIGI International (T) Limited, ambayo ni mwagizaji na msambazaji mkubwa wa mbolea ya mboji asilia aina ya Erth Food kutoka Marekani, inasema mbolea hiyo ndiyo mkombozi wa mkulima wa Tanzania kwa kuwa inatengenezwa kwa kutumia taka za shamba zisizo na kemikali ambapo inasaidia kurudisha udongo uliochoka kurudi katika hali yake ya asili; inatumika kwa mazao ya aina zote hata maua, miti na nyasi; inakaa na unyevunyevu muda mrefu; ni rafiki mkubwa wa mazingira; hutakiwi kuchanganya mbolea hii na mbolea nyingine za kemikali; mazao unayolima kutumia mbolea za asili ni bora sana na huchukua muda mfupi kukomaa; na zaidi, ukitumia mboji hutakuwa na haja ya kuhama shamba kwa sababu ardhi itakuwa na rutuba yake ya asili.

Hata hivyo, Tanzania bado haijafikia lengo la kuuza bidhaa za kilimo hai katika masoko ya Ulaya, Marekani na Japan kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ya wakulima kukosa elimu ya kilimo hicho kama alivyopata kusema Mkurugenzi wa kampuni ya Tanzania Zanzibar Organic Producers Limited (TAZOP), Bw. Khamis Issa Mohamed, wakati wa kongamano la wadau wa mazao ya kilimo hai nchini lililofanyika mwaka 2006 katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha kilimo (SUA).
Alisema wakulima wengi nchini hawana elimu ya kutosha kuhusu kilimo hicho pamoja na mtaji wa kuwawezesha kulima kilimo hai jambo linalokwamisha Tanzania kuuza bidhaa nyingi katika masoko ya Ulaya na Marekani.
Akatoa mfano wa kampuni yake ambayo mwaka 2005 ilikuwa na zabuni ya tani 200 za viungo mbalimbali kama hiliki, tangawizi, mdalasini, bizari, maganda ya machungwa na limao kupeleka nchini Ujerumani lakini ilishindwa kufikia lengo na badala yake iliuza tani 71 tu kwa kipindi hicho na kuingiza jumla ya dola za Kimarekani 192,000.

Hata hivyo, serikali inatakiwa kuongeza juhudi zaidi katika kuhamasisha wananchi waendeleze kilimo hai, ambacho ni endelevu na rafiki wa mazingira, ili kiwanufaishe zaidi kwani mazao yatokanayo na kilimo hicho yana uhakika wa soko ulimwenguni tofauti nay ale yanayotumia mbolea za kemikali.

Kukaa kimya kwa serikali kunamaanisha kwamba hata wadau wanaojitokeza kushabikia kilimo hai nchini watakata tamaa, kwani hata mbolea asilia wanazoziagiza kutoka nje ama kuzitengeneza zinakosa soko kutokana na wakulima kutokuwa na elimu na maafisa kilimo kugoma kuhamasisha utumiaji wa mbolea hizo kwa maelezo kwamba hawajapewa maagizo kutoka wizarani.

Kama kweli tunataka kujikomboa kupitia kilimo, kwa kweli hatuna budi kutumia zaidi kilimo hai ambacho pia kinaweza kutuepusha na migogoro ya ardhi kama inayojitokeza sasa baina ya wakulima na wafugaji.

Mwisho.

No comments:

JUST ANOTHER THOUGHT

JUST ANOTHER THOUGHT

A person asked God, “What surprises you most about mankind?”

And God answered,
“That they loose their Health to make money and they loose their money to restore their Health.

That by thinking anxiously about the future, they forget the present, such that they live neither for the present nor the future.

That they live as if they will never die and they die as if they had never lived.….”

BECAUSE I'M A MAN...

Because I’m a man, when one of our appliances stops working I will insist on taking it apart, despite evidence that this will just cost me twice as much once the repair person gets here and has to put it back together.

Because I’m a man, I don’t think we’re all that lost, and no, I don’t think we should stop and ask someone. Why would you listen to a complete stranger I mean, how the hell could he know where we’re going?

Because I’m a man, there is no need to ask me what I’m thinking about. The answer is always either sex or football, though I have to make up something else when you ask, so don’t.

Because I’m a man, I do not want to visit your mother, come visit us, or talk to her when she calls, or think about her any more than I have to. Whatever you got her for mother’s day is okay, I don’t need to see it. And don’t forget to pick up something for my mommy, too!

Because I’m a man, I am capable of announcing, “one more beer and I really have to go”, and mean it every single time I say it, even when it gets to the point that the one bar closes and my buddies and I have to go hunt down another. I will find it increasingly hilarious to have my pals call you to tell you I’ll be home soon, and no, I don’t understand why you threw all my clothes into the front yard. Like, what’s the connection?

Because I’m a man, you don’t have to ask me if I liked the movie. Chances are, if you’re crying at the end of it, I didn’t.

Because I’m a man, yes, I have to turn up the radio when Bruce Springsteen or The Doors comes on, and then, yes, I have to tell you every single time about how Bruce had his picture on the cover of Time and Newsweek the same day, or how Jim Morrison is buried in Paris and everyone visits his grave. Please do not behave as if you do not find this fascinating.

Because I’m a man, I think what you’re wearing is fine. I thought what you were wearing five minutes ago was fine, too. Either pair of shoes is fine. With the belt or without it looks fine. Your hair is fine. You look fine. Can we just go now?

Because I’m a man and this is, after all, the 90’s, I will share equally in the housework. You just do the laundry, the cooking, the gardening, the cleaning, and the dishes. I’ll do the rest.

A SIMPLE GUIDE TO LIFE

1. Follow your dream! Unless it’s the one where you’re at work in your underwear during a fire drill.

2. Always take time to stop and smell the roses and sooner or later, you’ll inhale a bee.

3. Do not walk behind me, for I may not lead. Do not walk ahead of me, for I may not follow. Do not walk beside me, either. Just leave me alone.

4. If you don’t like my driving, don’t call anyone. Just take another road. That’s why the highway department made so many of them.

5. If a motorist cuts you off, just turn the other cheek. Nothing gets the message across like a good mooning.

6. When I’m feeling down, I like to whistle. It makes the neighbor’s dog run to the end of his chain and gag himself.

7. It’s always darkest before dawn. So if you’re going to steal the neighbor’s newspaper, that’s the time to do it.

8. A handy telephone tip: Keep a small chalkboard near the phone. That way, when a salesman calls, you can hold the receiver up to it and run your fingernails across it until he hangs up.

9. Each day I try to enjoy something from each of the four groups: the bonbon group, that salty-snack group, the caffeine group and the “What ever-it-is-the-tinfoil-in-the-back-of-the-fridge”.

10. Into every life some rain must fall. Unusually when your car windows are down.

11. Just remember: You gotta break some eggs to make a real mess on the neighbor’s car!

12. When you find yourself getting irritated with someone, try to remember that all men are brothers and just give them a noogie.

13. This morning I woke up to the unmistakable scent of pigs in a blanket. That’s the price you pay for letting the relatives stay over.

14. It’s a small world. So you gotta use your elbows a lot.

15. Keep your nose to the grindstone and your shoulder to the wheel. It’s a lot cheaper than plastic surgery.

16. This land is your land. This land is my land. So stay in your land.

17. Love is like a roller coaster: When it’s good you don’t want to get off, and when it isn’t, you can’t wait to throw up.

DEDICATION TO YOUNG PEOPLE

Youth is a time of hope. Also of uncertainty. But for a person who is young and healthy, uncertainty just means a challenge. It is important to be positive. First of all about yourself. But also about your family and your people. As a unique person and each human being are unique, you have enormous potential. Because you have so much potential, people may sometimes feel negatively challenged by that potential and try to undermine it.

You have to fight for your right to make your place in society. To do that you have to use all the chances given you now to be a positive element in whatever situation you find yourself in, in future. So, it may be necessary to be a ‘rebel in reverse’ as it were. That takes real courage, to set your goal and stick to it. You choose your crowd. You exercise your right to choose.
Don’t lose your freedom for the sake of anyone. Real freedom, freedom to choose the right thing, the best for you.

Always bear a few things in mind while exercising your right to choose.

* Never take a decision when you are in a fit of anger or depression.
* Never take a decision when you are emotionally high.
* Why should fads or the decision of the group tie you down?
* What are you?
* What do you want tomorrow to be for you?

No matter how strong the group decision may be, you must think and make your decision. Many times it is necessary to consult before taking a decision. Go to someone whose life you admire, not necessarily the person you like most, but the person who is whole, who is one person, wherever she or he is and whatever she or he does.

* Remember that there is always tomorrow, and tomorrow is hope. Very few things are ‘written in stone’. Most of the mistakes we make can be rectified. They can be corrected. Problems have a solution, and each new day is a new start, a new chance, a New Hope. Indeed the youth are our hope you are our future.

Also remember that your parents love you unconditionally, you have their support and want the best in life for you ¨

COSTA VICTOR NAMPOKA

Mguu ulivyokatisha ndoto za kucheza soka Ulaya

DANIEL MBEGA
Dar es Salaam

NI majira ya saa 5.20 hivi asubuhi, niko hapa Ukonga-Banana nikiwania kupanda daladala la kwenda kwenye kitongoji cha Kitunda-Kibeberu, moja ya vitongoji vinavyokua kwa kasi hapa jijini Dar es Salaam.
Sijui ni umbali gani kutoka hapa, hivyo namuuliza dereva ambaye nimeketi naye pembeni yake. Ananiambia ni mwendo kama wa dakika 15 tu hivi. Nashusha pumzi kwa kujua kwamba kumbe si mbali sana kama nilivyofikiria.
Nawasili kwenye kitongoji cha Kibeberu, ambako ndiko magari yanakogeuzia, na bila kupoteza muda nampigia simu mwenyeji wangu kwamba tayari nimeshafika. Namhurumia huko aliko kama ataamua kuja kunipokea, lakini nafarijika anaponiambia kwamba nimuulize mtu yeyote hapo kituoni atanileta.
Watoto wawili wanajitolea kunipeleka nyumbani kwa mwenyeji wangu, ambaye namkuta akiwa kajilaza kwenye kochi akizungumza na rafiki zake wawili waliomtembelea. Anapenda kuketi vizuri, lakini hali haimruhusu.
“Poleni jamani kwa safari ndefu!” ndivyo anavyoanza kusema huyu mwenyeji wangu, ambaye si mwingine zaidi ya mlinzi mahiri wa timu ya soka ya Taifa, Taifa Stars, pamoja na klabu ya Simba, Costa Victor Nampoka ‘Nyumba’. Anajaribu kuuweka vyema mguu wake wa kulia ambao bado umefungwa bandeji gumu (POP) baada ya kuvunjia mazoezini takribani mwezi mmoja na nusu uliopita.
“Hakuna shaka, Dar es Salaam ni moja na hakuna sehemu unayoweza kusema ni mbali,” namjibu kumpa matumaini.
“Hapana! Pamoja na ukweli kwamba mkoa kazini, lakini naamini uamua kufunga safari mpaka kuja kuniona ni jambo kubwa sana. Mngeweza hata kuniuliza maendeleo yangu kwa njia ya simu. Sina budi kushukuru kwa kuja kunijulia hali,” anasema.
Mara anaingia dada mmoja mweupe hivi ambaye anaketi pamoja na Costa kwenye kochi moja. Costa mwenyewe anamtambulisha kwamba ndiye mkewe, Dina, ambaye wamebahatika kuzaa naye watoto wawili; Victor Costa mwenye miaka miwili na Rio Costa mwenye mwaka 1.5. Anatukaribisha.
Anapoondoka namwambia ni jambo la kawaida kuwatembelea wagonjwa, na katika suala lake yeye ni mmoja wa watu waliotoa mchango mkubwa katika timu ya taifa ya soka ambayo sasa iko katika nafasi nzuri ya kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika mwakani ikiwa tu itashinda mechi yake ya mwisho.
“Nashukuru kusikia hivyo, lakini sura zinazokuja hapa daima ni zile nilizozizowea, yaani marafiki zangu na wachezaji wenzangu wa klabu ya Simba, labda na viongozi wa Simba,” anasema kwa huzuni.
“Una maana kwamba viongozi wa timu ya taifa na hata TFF huwa hawakutembelei?” nauliza.
Anasema tangu alipoumia siku tatu kabla ya Taifa Stars kupambana na Zambia katika mechi ya kirafiki na kupelekwa Muhimbili na daktari wa timu Shecky Mngazija, hajatembelewa wala kujuliwa hali hata kwa simu na kiongozi yeyote yule wa chombo hicho cha juu cha soka nchini.
Anaongeza kwamba, ni wachezaji wenzake wa Simba ndio baadhi yao huwa wanawasiliana naye pamoja na viongozi na marafiki wa klabu ambao wameonekana kumjali vya kutosha kiasi cha kutuma gari kila siku katika mechi zote ambazo Simba ilicheza kwenye hatua ya Sita Bora ya Ligi ya Mpito hadi fainali.
“Kwa kweli viongozi wa klabu yangu wananijali sana na sina budi kuwashukuru,” anasema. Kama vile amekumbuka kitu, anasema anamshukuru pia mtu mmoja wa Benki ya NMB anayeitwa Kajura (Imani Kajura ambaye ni Meneja Masoko).
“Huyu jamaa baada ya kutoa zawadi za shilingi 500,000 kwa kila mchezaji kutokana na timu ya Taifa kushinda kule Burkina Faso, alinipigia simu kuniambia nilitakiwa kwenda kusaini fomu za akaunti. Nikamwambia sina hata pesa ya nauli na kwa jinsi ninavyoumwa nisingeweza kupanda daladala, lakini akaniambia nichukue teksi nay eye angelipa. Namshukuru sana,” anasema.
Hata hivyo, amewaasa wachezaji wengine; wa klabu na hata timu ya taifa, kwamba pindi watakapoumia na kushindwa kujuliwa hali na viongozi wao wasife moyo bali hiyo iwe changamoto kwao kufanya vizuri watakaporejea uwanjani.
“Binafsi sina kinyongo na yeyote. Naomba Mungu nipone nirejee uwanjani, ikibidi niliwakilishe taifa langu, kwa sababu natambua kwamba timu ya Taifa ni ya Watanzania wote wala si ya mtu mmoja. Naamini Watanzania milioni kadhaa wako pamoja na mimi na hata walipojua kwamba nimeumia walinitumia meseji za pole zaidi ya 3,000, hata sijui walikoipata namba yangu,” anasema.

Kuvunjika mguu
Costa anasema kwamba walikuwa kwenye mazoezi kama kawaida kwenye uwanja wa Karume, akauzuia mpira bila kumkwatua ama kukwatuliwa, kisha akaserereka.
“Ghafla nikasikia maumivu makali sana, ikabidi wajaribu kuniganga pale, lakini yalipozidi wakanikimbiza Muhimbili. Huko nikaambiwa kwamba nimevunjika mfupa mdogo wa mguu wa kulia. Sikuwa na jinsi, wakanifunga hogo (bandeji gumu – POP) na kusema kwamba nirudi baada ya wiki sita,” anasema kwa majonzi.
Anasema kwamba, baada ya kutolewa kwa bandeji hilo ndipo atakapojua kama atakuwa nje ya uwanja kwa muda gani, kwani mpaka sasa hajaanza hata kuukanyangia mguu huo.
Akasema kuvunjika mguu kumemnyima nafasi ya kuliwakilisha taifa, na zaidi kumechelewesha kutimia kwa ndoto zake kwani pengine hivi sasa angeweza kuwa Afrika Kusini kujaribu kucheza soka ya kulipwa akiwa njiani kwenda cheza Ulaya.
“Kuna wakala mmoja ambaye kwa muda mrefu sasa amekuwa akinufuatilia, yuko Afrika Kusini, na alikwenda Burkina Faso kunitazama, lakini mimi sikuwepo. Ilikuwa niende Afrika Kusini kufanya majaribio na naamini ningewea kufanikiwa,” anasema mchezaji huyo.
Anasema kwamba, alikuwa na matumaini ya kufuzu kwa sababu soka ya Afrika Kusini haina tofauti na ya huku, tena hakuwa mgeni baada ya kucheza kwa muda nchini humo miaka mitatu iliyopita.
“Wanachotuzidi kule ni promosheni, televisheni zinajitahidi sana kuonyesha mpira hata wa daraja la tatu, na hiyo inamsaidia mchezaji kutazama na kuona wapi alipokosea ili kujirekebisha, ama afanye nini kuongeza jitihada,” anasema.
Anaongeza kwamba alishindwa kuendelea kucheza huko kwa sababu klabu aliyokuwa akiichezea wakati ule ya Marlasburg (Tembas) iliyokuwa daraja la kwanza mwaka 2005 ikiwa chini ya kocha wa zamani wa Simba Trott Moloto, iliinunua klabu moja iliyokuwa ligi kuu. Ikabidi wachezaji wa timu hizo wachekechwe, na majungu ndipo yakaibuka ambapo Moloto, ambaye ndiye aliyemfanyia mpango wa kwenda huko, akamgeuka. Ikabidi afungashe virago kurejea.
Hata hivyo, anasema kwamba ndoto zake bado hazijafutika, kwani anaamini anaweza kucheza Ulaya bila matatizo yoyote, na zaidi anasema angependa siku moja avae ‘uzi’ wa Manchester United akicheza pembeni ya Rio Ferdnand ambaye uchezaji wake unamvutia kiasi cha kumwitia mwanawe mdogo jina hilo kutokana na kumhusudu.
Akizungumzia nafasi ya Taifa Stars kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika mwakani, Costa (25) ambaye ni mtoto wa nne katika familia ya watoto watano wa mzee Victor Nampoka – wawili wanawake na watatu wanaume, anasema kwamba nafasi ipo, lakini mechi ya mwisho dhidi ya Msumbiji ni ngumu sana.
“Ile mechi ni kama fainali na inabidi maandalizi ya nguvu yafanyike pengine kuliko mechi zote zilizotangulia. Msumbiji ni wazuri sana kuliko hata Burkina Faso, na ina nafasi ya kufuzu ikiwa itashinda na Senegal wakafungwa, hivyo Watanzania tusibweteke bali tujiandae vizuri,” anasema huku akisikitika kwamba anaweza kuikosa mechi hiyo pia ikiwa ataambiwa apumzike.
Akizungumzia kuhusu maendeleo ya soka, mlinzi huyo anasema kwamba hakuna kitakachoinua zaidi ya soka la vijana, na kuongeza kwamba mashindano ya Copa Coca Cola yawe chachu wa klabu na wadau mbalimbali kuanza kuibua vipaji.
“Kule Brazil tulikokwenda kuna taasisi ya soka ya watoto wadogo. Watoto wanatoka nchi mbalimbali kwenda kufundishwa mpira, na wazazi wao wanalipia wastani wa dola 1,500 kwa mwezi ili watoto wao wajue mpira. Tusione wenzetu wamepiga hatua tukadhani kwamba ni miujiza, wamewekeza.
“Watanzania wanapaswa kuunga mkono juhudi za maendeleo ya soka ya vijana, kuanzia kwa wazazi, ambao wanapaswa kuwapa ‘sapoti’ watoto wao ikiwa ni pamoja na kuwapatia vifaa vya michezo na nauli ya kwenda mazoezini,” anaongeza.
Costa aliyemaliza elimu ya msingi mwaka 1994 Kinondoni Hananasif, jijini Dar es Salaam na kuungana na maelfu ya watoto ambao hawakufanikiwa kuchaguliwa kujiunga na sekondari, amewashauri wachezaji kuachana na anasa na kwamba wawe na malengo kama kweli wanataka kupiga hatua katika mchezo huo.
“Sijafanikiwa sana, lakini niseme ukweli kwamba nimejiepusha na mambo mengi. Sivuti sigara wala bangi, halafu niliacha kitambo kunywa pombe, tena basi nilikuwa nikinywa bia mbili ama tatu tu, lakini sasa sitaki kabisa nahitaji kukazana kwenye mpira ambao pekee ndio mwokozi wangu katika maisha,” anamalizia.

Wasifu:
Jina: Costa Victor Nampoka
Kuzaliwa: Oktoba 11, 1982, Dar es Salaam.
Umri: 25

Klabu za awali:
Five Star Kinondoni, Mkunguni FC Ilala, Eleven FC Buguruni, Saddam FC na International FC za Kinondoni.
Taifa Jang’ombe – Zanzibar (1998 – 1999)
Forodha Zanzibar (2000 – 2001)
Mtibwa Sugar (2002)
Simba (2003 – 2004)
Marlsburg – Afrika Kusini (2005)
Simba (2006 – mpaka sasa).