Friday, August 20, 2010

Shigongo kiungo sahihi maendeleo ya Buchosa
Na Mwandishi Wetu
ILIMCHUKUA muda mrefu kuamua kukubali ombi la wananchi wa Buchosa. Kwa kitambo kirefu walimtaka awe mbunge wa jimbo lao. Waliamini katika maono yake, nidhamu aliyonayo, sifa aliyojaaliwa ya uchapakazi, moyo wa kujitolea kwa wengine na upendo kwa watu wote.
Mwalimu wa Kimataifa wa somo la ujasiriamali, Eric James Shigongo ameamua kusikia la wakuu. Tofauti na vipindi vilivyopita, awamu hii ameona si vema kuendelea kuchelewa kutii ombi la wazee wa Buchosa na wananchi wengine wanaomuamini na kumpenda. Amechukua fomu ya kugombea ubunge, na sasa yupo uwanja wa mapambano.
Shigongo ambaye ni kada wa siku nyingi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) aliye pia Mwenyekiti Mstaafu wa Kamati ya Ukimwi katika Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), anapoamua kugombea Buchosa, anageuza tafsiri ya “mti ukirefuka sana, hutoa faida kwa jirani kuliko kwa mmiliki.”
Umepanda mti unarefuka mno. Matokeo yake kivuli kinakwenda nyumba ya jirani. Shigongo anaona hilo siyo sawa. Kwa umaarufu wake na jinsi alivyojitawanya kitaifa angeweza kugombea majimbo mengine na kushinda lakini kwa kutambua alipotoka, anarudi Buchosa alikozaliwa.
Je, unadhani Shigongo anahitaji ubunge tu? Kama unafikiria hivyo, hapo utakuwa umekosea. Tena upo mbali mno na ukweli! Kilichompeleka kugombea Buchosa ni kurejesha kivuli nyumbani. Ana wito wa shida walizonazo wananchi.
Alizaliwa hapo, anajua matatizo ya ndugu zake. Alishiriki miradi mingi ya kusaidia jimbo lake, lakini anaamini akiwa mwakilishi wa jimbo hilo ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, atasaidia kuharakisha maendeleo. Atakuwa msaada wa Mwenyekiti wa CCM Taifa, Jakaya Kikwete katika kutekeleza ilani ya chama.
“Sigombei ubunge kutaka gari, umaarufu au uwaziri. Nimevutwa na shida walizonazo wananchi wa Buchosa. Nina nia ya dhati ya kushirikiana na Rais Kikwete katika kuwaletea maendeleo ya kweli wananchi wa Buchosa,” anasema Shigongo anapowasha taa kuomba njia ya kupita kuelekea bungeni, Dodoma.
Anasema: “Nimezaliwa Buchosa na kukulia hapo. Nawajua ndugu zangu wa Buchosa, nazitambua shida zao. Wanahitaji mtu makini ambaye anaweza kuwaongoza. Ambaye atarudisha umoja wao ambao kwa muda mrefu umetoweka. Kuna makundi kwa sababu za kisiasa, mimi nataka nizimalize tofauti zote halafu tushirikiane kuleta maendeleo.
“Sitaki kusema uongo, niwadanganye wananchi kwamba mimi ni msomi mkubwa au nina degree (shahada ya chuo kikuu). Siwezi kujivika sifa ambazo sina, ila nina uwezo wa kusimamia kitu kutoka sifuri hadi kupanda juu kabisa kama ambavyo maisha yangu ya kijamii na kibiashara yanavyojifafanua.”
Hata hivyo, Shigongo anatoa mwanga kwa wana Buchosa kuchagua kilicho bora kulingana na upeo wao. Anasema: “Siingii kwenye kinyang’anyiro cha ubunge Buchosa kufanya siasa za chuki. Hata siku moja sitozua kitu kumchafua mtu, wala sitothubutu kutukana mtu.
“Nitaeleza dhamira yangu ya kuleta maendeleo na umoja kwa ndugu zangu. Kila mara natembelea nyumbani kwetu na kuona watu wanavyotaabika. Kwa miaka yote, Buchosa hatuna hata high school (shule ya juu) hata moja. Vijana wa kike wanashindwa kuendelea na masomo, matokeo yake wanakwenda kutafuta unafuu visiwani.
“Huko nako siyo pazuri. Wengi wanaambukizwa virusi vya ukimwi na kugeuka mzigo kwa familia zao. Tiba ya hilo ni kujenga shule za juu na za ufundi. Vijana wasome na kujifunza kujitegemea. Kama wana Buchosa watanipitisha, nitashirikiana nao kupata ufumbuzi wa kudumu wa matatizo hayo.”
Kwanini Buchosa? Shigongo analijibu hilo: “Nikiwa Dar es Salaam, naishi Mbezi, kwahiyo ningeweza kugombea Kawe. Mwanza mjini, nyumbani kwangu ni Capripoint, kwahiyo ningeweza kusimama na kugombea Nyamagana. Wazazi wangu wanaishi Nyakato, ningeweza kugombea Ilemela.
“Kote huko naishi vizuri na watu, wananipenda na wao wananipenda. Sina kawaida ya kuwa na matatizo na watu, lakini akili yangu haipo kwenye jimbo lolote zaidi ya Buchosa. Mimi ni mtu wa Buchosa. Hata nikiwa naishi Marekani, nikifa maiti yangu itarudishwa Buchosa.
“Ninavyoishi na familia yangu kila siku, nawafundisha watoto wangu watambue kuwa wao nyumbani kwao ni Buchosa. Hii ndiyo sababu iliyonifanya nisichague jimbo lolote, badala yake nirudi nyumbani kwetu, na kama ni mafanikio basi niyajenge kwenye ardhi niliyozaliwa.
“Na kwa sababu Buchosa ni nyumbani, sitokubali siasa za chuki zichukue nafasi na kuongeza uadui ambao umekuwepo kwa muda mrefu. Makundi ya mwanasiasa huyu na yule, mimi nataka kumaliza matabaka, lakini nawataka watu wa Buchosa kufanya uchaguzi wa sahihi.
“Wamchague mtu ambaye anaweza kumaliza uadui uliopo kwa muda mrefu. Hata kama siyo mimi, basi watupe kiongozi ambaye hatotufanya tujute kwa miaka mitano ijayo. Mimi najiamini kwa sababu nina dhamira ya dhati. Uongozi ni uwezo, moyo na hekima kutoka kwa Mungu.”
Shigongo anasema kuwa wananchi wa Buchosa wana kila sababu ya kumuamini kwa sababu amejaliwa karama na Muumba ya kuongoza na kusimamia vitu. Anaeleza kwamba nguvu iliyomhamisha kutoka katika maisha duni kwenye kijiji cha Bupandwa, Buchosa wilayani Sengerema ni hoja kuu ya kukubali maono yake.
Kada huyo wa CCM ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Global Publishers & General Enterprises Ltd, inayochapisha magazeti mbambali maarufu nchini, anasema kuwa kutanuka kibiashara kwa kampuni yake mpaka Los Angeles, California, Marekani ni ishara ya wazi kwamba anaweza kuongoza.
Anasema kuwa ndoto zake ni kuona vijana wengi zaidi wa Buchosa wanapata muamko wa kusaka maendeleo yao. Anaeleza kwamba hilo halitowezekana endapo hawatopata mtu anayewapenda, atakayewatetea, kuwapigania na kuwapa muongozo ambao ni taa ya mafanikio.
Shigongo anaeleza kwamba atakapokuwa mbunge wa Buchosa, atakuwa taa ya vijana kuwa wajasiriamali. Atahakikisha anautumia uzoefu wake kama tiba kwa wengine. Anasisitiza: “Nimezunguka sehemu mbalimbali nafundisha watu kuwa wajasiriamali.
“Nimetoa semina nyingi nchini. Naandika makala ya Waraka wa Shigongo kwenye gazeti la Ijumaa Wikienda ili kuwasaidia watu kujikwamua kiuchumi. Hivi karibuni nilikuwa Minnesota, Marekani ambako nilizungumza na Watanzania wanaoishi nchini humo na kuwaambia umuhimu wa kuja nchini tujenge nchi.
“Uzoefu wangu huo wa kibiashara na kufundisha ujasiriamali, naamini ni lulu itakayorahisisha maendeleo ya mtu mmoja mmoja kwa wakazi wa Buchosa na jimbo letu kwa jumla. Naomba waniamini ili tutumie fursa tulizonazo ili kusaidia kizazi cha sasa na kijacho jimboni kwetu.
“Buchosa tuna msitu mkubwa. Tuna ziwa na ardhi yenye rutuba kuliko sehemu yotote ya mkoa wa Mwanza. Endapo wana Buchosa wataniamini na kuniteua kuwa mgombea kwenye chama changu na baadaye kunichagua kuwa mbunge, naamini tunaweza kuifanya Buchosa kuwa kitovu cha uchumi Mwanza.”
Shigongo ambaye alijipatia umaarufu mkubwa nchini kutokana na umahiri wake wa kuandika riwaya zinazochapishwa na magazeti pendwa nchini na kuvutia wasomaji wengi, anawaonya wakazi wa Buchosa kutomhukumu kwa sababu hana shahada ya chuo kikuu.
Mwandishi huyo wa vitabu vya Machozi na Damu, Siku za Mwisho za Uhai Wangu na Rais Anampenda Mke Wangu, anawakumbusha kauli ya mzee mmoja anayeitwa Matahekumi ambaye alisema akiwa kwenye kijiji cha Nyakalilo, Buchosa kuwa Chama cha Ushirika cha Nyanza kilikufa kwa sababu ya kuwaamini wasomi.
Shigongo anasema kwa kumnukuu Matahekumi: “Nyanza ililelewa na wazee ambao hawakuwa na elimu ya darasani, lakini kwa sababu walikuwa na nidhamu ya kuongoza, chama kilikua mpaka kikafikia hatua ya kutaka kununua ndege.
“Lakini chama kilipokabidhiwa kwa wasomi kilikufa hapo hapo.” Baada ya mfano huo, Shigongo anasema: “Ni vizuri wana Buchosa wakaniamini. Elimu ya kuwaongoza ninayo, tena kubwa mno ambayo inaweza kuwasaidia. Kuhusu shahada ya Chuo Kikuu, wachukue kauli ya kizalendo ya mzee Matahekumi.”
Shigongo mbali na ujasiriamali, pia alipata umaarufu mkubwa pale alipoanzisha na kusimamia kampeni mbalimbali za kusaidia jamii ya watu wenye matatizo, wakiwemo wagonjwa waliokata tamaa na kuwawezesha kupata tiba bora nje ya nchi, hasa India na kupona kabisa.
Akiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ukimwi katika UVCCM, Shigongo aliendesha kampendi maalum ya kupiga vita ugonjwa huo. Alihakikisha kila mwaka anaandaa kauli mbiu na maonesho maalum katika mikoa mbalimbali nchini, yenye sura ya kupambana na VVU kila Desemba Mosi ambayo kwa kawaida ni kilele cha Siku ya Ukimwi Duniani.
Mwaka 2005, wazee na wananchi wengine wa Buchosa walimtaka agombee, lakini kutokana na kukabiliwa na matatizo ya kifamilia, aliamua kumpa ushirikiano mbunge anayemaliza muda wake, Samuel Chitalilo.
Hata hivyo, uamuzi huo uliibua hasira kwa wazee, wazazi pamoja na wakazi wengine wa jimbo hilo ambapo mwaka 2006, Shigongo alilazimika kutoa waraka maalumu uliojaa ukurasa mzima kwenye gazeti la Uwazi, akiomba radhi na kuahidi kutowaangusha kwenye Uchaguzi Mkuu 2010.
Shigongo, alizaliwa miaka 40 iliyopita kwenye kijiji cha Mwangika, Buchosa wilayani Sengerema Mwanza. Ni baba wa familia yenye mke mmoja, Veneranda na watoto watatu, Andrew, Samuel na Baraka. Ni mkulima pia, anamiliki shamba la ekari 250 Kiwangwa Bagamoyo na anayo kampuni ya matrekta.
Mwenye kisu kikali ndiye atakula nyama Songea Mjini 2010

* Dk. Nchimbi atamba amefanya mengi, ahukumiwe kwa mafanikio
* Asema ni haki kwa yeyote kugombea, lakini Mbunge ni mmoja tu

Na Mwandishi Maalum, Songea

“Usimpe maskini samaki, mfundishe jinsi ya kuvua!” Huu ni msemo wa Wahenga ambao kwa hakika una mantiki kubwa katika maisha yetu ya kila siku. Ukimpa samaki atakula, atashiba, lakini kesho njaa itamuuma tena, atakufuata, hivyo bora umfundishe uvuvi ili njaa ikimuuma hatavua wa kula pekee bali na wa akiba.
Tafsiri hii ndiyo inayoonekana kutumika kwa Mbunge wa Songea Mjini (CCM) Dk. Emmanuel John Nchimbi, baada ya kufanikisha ujenzi wa Shule ya Sekondari Mkuzo ambayo itakuwa inachukua wanafunzi wa kidato cha tano na sita.
Shule hiyo iliyojengwa katika eneo la Msamara, Kata ya Bombambili katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mjini, tayari imekwishakabidhiwa serikalini tangu mwezi Mei 2010 ili kusaidia kupunguza tatizo la wanafunzi kukosa nafasi za kujiunga na masomo ya kidato cha tano, hivyo kuwakomboa kielimu wananchi wa Songea.
Shule hiyo imejengwa kwa gharama ya shilingi milioni 112 bila ya michango ya wananchi na ina madarasa 10 na jengo la utawala ambapo kwa sasa ina uwezo wa kuchukua wanafunzi 400 kwa wakati mmoja na itakapokamilika itakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi 800 kwa wakati mmoja.
Dk. Nchimbi anasema ameijenga shule hiyo kutokana na misaada aliyoipata kutoka kwa ndugu, marafiki zake na mshahara wake wa unaibu waziri wa miaka minne iliyopita.
Mbali ya kujenga mwenyewe shule hiyo, lakini pia maeneo mengine ambayo amechangia katika sekta ya elimu kuwa ni msaada wa fedha za ujenzi wa sekondari za kata zote 13 za Manispaa ya Songea vikiwa na thamani ya shilingi 141,398,000, kununua vitabu kwa ajili ya shule za sekondari binafsi na serikali vilivyogharimu shilingi milioni 30, na pia anawalipia ada wanafunzi 28 wa sekondari, wanafunzi 10 wa vyuo vya kawaida, na wanafunzi sita wa chuo kikuu, ambapo gharama zake ni jumla ya shilingi 11,900,200.
"Wananchi wenzangu leo nawakabidhi majengo mazuri ya sekondari hapa Mkuzo niliyoyajenga kwa zaidi ya milioni 112/=. Kwa fedha hizi ningeweza kujenga hoteli nzuri ya kisasa kwenye uwanda mzuri wa Matogoro na kuzifungua kifahari, lakini ingekuwa kwa maslahi yangu na familia yangu, lakini kwa kuwa nawapenda nimeamua kuwekeza kwenye elimu ya watoto wetu wote wa Songea," alisema Nchimbi siku ya kukabidhi shule hiyo.
"Leo ni siku muhimu katika manispaa yetu mtakumbuka miaka minne iliyopita CCM iliahidi kuwa tuitajenga sekondari kila kata ni faraja kubwa jambo hilo tumelikamilisha, matokeo ya kujenga shule yapo wazi kwani uwekezaji wa elimu ni muhimu kuliko yote," anasema Dk. Nchimbi na kuthibitisha kwamba elimu bora ni sawa na kumfundisha mtu uvuvi badala ya kumpatia samaki kwa njaa ya siku moja.
Dk. Nchimbi anasema pamoja na mafanikio hayo lakini bado kuna changamoto nyingi katika sekta hiyo ya elimu jimboni kwake ambapo alizitaja changamoto hizo kuwa ni upungufu wa walimu, vifaa, kuboresha majengo na miundombinu ya shule za msingi, walimu kulipwa haki zao kwa wakati na kujenga chuo kikuu mjini Songea ambacho kitasaidia wananchi wa mkoa wa Ruvuma kujiendeleza zaidi kielimu.
Anasema iwapo wananchi wataendelea kumpatia ushirikiano atasaidiana nao kujenga chuo kikuu katika Manispaa hiyo kwani kwa sasa ndoto yake kubwa ni kuhakikisha kuwa watoto wote wenye uwezo wa kusoma wanaenda shule ili kuongeza idadi ya wasomi katika mkoa wa Ruvuma, ahadi ambayo ilipokelewa kwa shangwe na wazazi pamoja na wanafunzi.
Wananchi wa Jimbo hilo bado wanalalamikia kero mbalimbali zinazowakabili na wamemtaka mbunge wao aongeze juhudi za kutatua kero hizo katika sekta ya maji, umeme, afya, elimu na barabara.
Lakini Dk. Nchimbi anasema kwa kipindi cha miaka minne na nusu ya uwakilishaji wake amejitahidi kutekekeza ahadi zake muhimu alizoziahidi, ambazo anasema zilikuwa kikwazo kwa maendeleo ya wapiga kura wake katika sekta ya elimu, afya na barabara, ingawa amewaomba wapiga kura wake wawe na subira kwani kero zao anazitambua na ameanza kuzitatua ingawa anakiri kuchelewa kuzitatua.
Ujenzi wa shule za sekondari za kata uligharimu fedha nyingi, ambapo wananchi walichanga jumla ya shilingi milioni 60 na Manispaa ikachangia shilingi milioni 70, hivyo kufanya kata zote kuwa na shule.
Jimbo hili la Songea Mjini lina jumla ya Kata 13 ambazo ni Matogoro, Mletele, Bombambili, Mshangano, Ruhuwiko, Subira, Ruvuma, Lizaboni, Majengo, Matarawe, Misufini na Mjini.
Katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu, wapo watu ambao wamekuwa wakisema kwamba huenda hizi ni mojawapo ya kampeni, jambo ambalo Dk. Nchimbi analikanusha na kusema kwamba ujenzi huwa hauchukui siku moja, bali ni mipango ya muda mrefu, hivyo lilikuwa mojawapo ya ahadi zake kwa wananchi na amelitekeleza.
Kauli hizi zimekuwa zikitolewa katika kipindi hiki ambacho vuguvugu la uchaguzi limepamba moto ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), ambapo katika jimbo hilo mbali ya Dk. Nchimbi anayetaka kulitetea, wamejitokeza watoto wa wanasiasa wakongwe nchini, Balozi Paulo Mhaiki na Nassor Hassan Moyo, ambao ni Oliver Mhaiki na Said Nassor Moyo.
Mhaiki, Katibu Mkuu wa Wizara ya Sheria na Katiba, anajivunia uzawa na ukazi mjini Songea, huku baadhi ya watu wakisema kwamba Dk. Nchimbi hakuzaliwa Songea na kwamba amejenga Mbeya.
Lakini hoja za aina hii ni za ubaguzi ambazo hazistahili kupewa nafasi, kwani Tanzania ni moja na masuala ya ukabila, udini hayastahili kupewa nafasi kwa sababu mwishowe zitakuja kuzuka hoja za “Huyu ni mtoto wa ukoo gani?” na mambo kama hayo.
Dk. Nchimbi anabainisha kwamba, ni haki kwa mwananchi yeyote mwenye sifa kugombea, kwani hata Katiba ya nchi inaeleza hivyo, lakini anaamini kwamba wananchi watamhukumu kwa mafanikio yake.
“Nimejitahidi kwa kadiri ya uwezo wangu, pamoja na majukumu mengi ya kiserikali niliyo nayo, hata hivyo huwezi kumridhisha kila mtu, na daima kero zote haziwezi kutatuliwa mara moja. Naamini nimefanya mengi na wananchi watakuwa mashuhuda.
“Wacha wajitokeze wengi kwa sababu ndiyo demokrasia, lakini naamini mwisho wa siku Mbunge atakuwa mmoja! Hili halina ubishi,” anabainisha Dk. Nchimbi ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.
Wachunguzi wa masuala ya siasa wanaona kwamba, nguzo pekee ya kuegemea ni kama kiongozi aliyechaguliwa na wananchi anawaletea maendeleo ama la, bila kujali anatoka mahali gani.
Ni wazi kwamba joto la uchaguzi jimboni humo limepanda kwa nyuzi nyingi, lakini wananchi ndio watakaopima mafanikio na kuamua kwa busara nani anayestahili kuwaongoza badala ya kuanzisha hoja zisizo na msingi.
Kwa sasa siasa chafu ndizo zinazotawala ndani ya jimbo la Songea Mjini, ambapo kuna kundi la mgombea mmoja lililodhamiria kumchafua mgombea mwenzake kwa kila hali na kuhakikisha anashindwa katika kura za maoni.
Kitendo cha kutumia mbinu za aina hiyo hakipaswi kufumbiwa macho, kwa sababu hakilengi kutumia demokrasia ya kweli bali hila za wazi, ambazo mwelekeo wake hautakuwa na matunda mazuri hata kama anayetumia mbinu hizo chafu ataingia madarakani.
Kwa upande wao baadhi ya wananchi wamesema kuwa kitendo cha Mbunge wao kuwajengea shule ni cha kuungwa mkono na wananchi wote wa manispaa hiyo kwani shule hiyo itawasaidia wananchi wote bila kujali itikadi za dini na siasa kupata elimu na wamewataka wenzao kuunga mkono jitihada za mbunge huyo.
Jacob Chidumule, mkazi wa Kata ya Matarawe, anasema kipindi cha uchaguzi kina mambo mengi, lakini lazima wananchi watumie busara wanapotaka mabadiliko ya maendeleo na siyo kufanya mabadiliko kwa shinikizo la watu wachache.
“Tunahitaji maendeleo, lakini siyo kukurupuka na kusema tunataka mabadiliko bila kutathmini mafanikio yaliyopatikana kwa yule tuliyemchagua. Binafsi naamini Nchimbi bado anastahili kutuwakilisha. Maendeleo yanaletwa kwa ushirikiano wa wote, viongozi na wananchi, na tusiwaachie viongozi pekee,” anafafanua Chidumule.
Naye Hassan Komba, mkazi wa Kata ya Bombambili, anasema kwamba CCM itafanya makosa ikiwa italeta mabadiliko ya lazima kwa mwakilishi, kwani wananchi bado wana imani na Mbunge wa sasa.
“Wakifanya mabadiliko ya ghafla, hakika wanaweza kujikuta wakilipoteza Jimbo kwa wapinzani. Tunaamini Mbunge wa sasa bado ana uwezo wa kuleta maendeleo. Hizi hoja za kazaliwa wapi anaishi wapi zisilete matabaka na hazijengi. Sote ni Watanzania na tunapaswa kuthaminiana kwa Utanzania wetu, tusije tukafikia mahali tukaanza kuulizana huyu ni mtoto wa nani?” anaonya Komba.
Felister Herman Haule, mkazi wa Kata ya Ruhuwiko, mewataka wananchi wenzake wa Manispaa ya Songea kumuunga mkono Mbunge wao kwa kushirikiana naye kwa vitendo ili kulipa shukrani kwa kuwakomboa kielimu kwani kitendo chake cha kujenga shule kitasaidia wananchi wengi kupata elimu na hivyo kuwa na wasomi ambao watasaidia kuleta maendeleo.
"Elimu ni msingi wa maendeleo yetu, Dk. Nchimbi amesababisha watoto wetu waende shule, ametoa fedha zake ili wananchi wake wajikomboe na tatizo la ujinga na umaskini hivyo wananchi tuache kubabaishwa na majambazi wa siasa tuchague viongozi ambao watatusaidia kujikomboa kielimu, kiuchumi na kulisaidia taifa letu katika nyanja mbali mbali za maendeleo,” anasema.
Fomu za kuwania Ubunge kwa upande wa Chama cha Mapinduzi (CCM) zinatarajiwa kuanza kutolewa Julai 19, mwaka huu, na kampeni ndani ya chama hicho zitaanza mapema mwezi Agosti.
Tusubiri tuone matokeo, lakini hakika mwenye kisu kikali ndiye atakayekula nyama Songea Mjini mwaka 2010!
SOURCE: DIRA YA MTANZANIA.

No comments:

JUST ANOTHER THOUGHT

JUST ANOTHER THOUGHT

A person asked God, “What surprises you most about mankind?”

And God answered,
“That they loose their Health to make money and they loose their money to restore their Health.

That by thinking anxiously about the future, they forget the present, such that they live neither for the present nor the future.

That they live as if they will never die and they die as if they had never lived.….”

BECAUSE I'M A MAN...

Because I’m a man, when one of our appliances stops working I will insist on taking it apart, despite evidence that this will just cost me twice as much once the repair person gets here and has to put it back together.

Because I’m a man, I don’t think we’re all that lost, and no, I don’t think we should stop and ask someone. Why would you listen to a complete stranger I mean, how the hell could he know where we’re going?

Because I’m a man, there is no need to ask me what I’m thinking about. The answer is always either sex or football, though I have to make up something else when you ask, so don’t.

Because I’m a man, I do not want to visit your mother, come visit us, or talk to her when she calls, or think about her any more than I have to. Whatever you got her for mother’s day is okay, I don’t need to see it. And don’t forget to pick up something for my mommy, too!

Because I’m a man, I am capable of announcing, “one more beer and I really have to go”, and mean it every single time I say it, even when it gets to the point that the one bar closes and my buddies and I have to go hunt down another. I will find it increasingly hilarious to have my pals call you to tell you I’ll be home soon, and no, I don’t understand why you threw all my clothes into the front yard. Like, what’s the connection?

Because I’m a man, you don’t have to ask me if I liked the movie. Chances are, if you’re crying at the end of it, I didn’t.

Because I’m a man, yes, I have to turn up the radio when Bruce Springsteen or The Doors comes on, and then, yes, I have to tell you every single time about how Bruce had his picture on the cover of Time and Newsweek the same day, or how Jim Morrison is buried in Paris and everyone visits his grave. Please do not behave as if you do not find this fascinating.

Because I’m a man, I think what you’re wearing is fine. I thought what you were wearing five minutes ago was fine, too. Either pair of shoes is fine. With the belt or without it looks fine. Your hair is fine. You look fine. Can we just go now?

Because I’m a man and this is, after all, the 90’s, I will share equally in the housework. You just do the laundry, the cooking, the gardening, the cleaning, and the dishes. I’ll do the rest.

A SIMPLE GUIDE TO LIFE

1. Follow your dream! Unless it’s the one where you’re at work in your underwear during a fire drill.

2. Always take time to stop and smell the roses and sooner or later, you’ll inhale a bee.

3. Do not walk behind me, for I may not lead. Do not walk ahead of me, for I may not follow. Do not walk beside me, either. Just leave me alone.

4. If you don’t like my driving, don’t call anyone. Just take another road. That’s why the highway department made so many of them.

5. If a motorist cuts you off, just turn the other cheek. Nothing gets the message across like a good mooning.

6. When I’m feeling down, I like to whistle. It makes the neighbor’s dog run to the end of his chain and gag himself.

7. It’s always darkest before dawn. So if you’re going to steal the neighbor’s newspaper, that’s the time to do it.

8. A handy telephone tip: Keep a small chalkboard near the phone. That way, when a salesman calls, you can hold the receiver up to it and run your fingernails across it until he hangs up.

9. Each day I try to enjoy something from each of the four groups: the bonbon group, that salty-snack group, the caffeine group and the “What ever-it-is-the-tinfoil-in-the-back-of-the-fridge”.

10. Into every life some rain must fall. Unusually when your car windows are down.

11. Just remember: You gotta break some eggs to make a real mess on the neighbor’s car!

12. When you find yourself getting irritated with someone, try to remember that all men are brothers and just give them a noogie.

13. This morning I woke up to the unmistakable scent of pigs in a blanket. That’s the price you pay for letting the relatives stay over.

14. It’s a small world. So you gotta use your elbows a lot.

15. Keep your nose to the grindstone and your shoulder to the wheel. It’s a lot cheaper than plastic surgery.

16. This land is your land. This land is my land. So stay in your land.

17. Love is like a roller coaster: When it’s good you don’t want to get off, and when it isn’t, you can’t wait to throw up.

DEDICATION TO YOUNG PEOPLE

Youth is a time of hope. Also of uncertainty. But for a person who is young and healthy, uncertainty just means a challenge. It is important to be positive. First of all about yourself. But also about your family and your people. As a unique person and each human being are unique, you have enormous potential. Because you have so much potential, people may sometimes feel negatively challenged by that potential and try to undermine it.

You have to fight for your right to make your place in society. To do that you have to use all the chances given you now to be a positive element in whatever situation you find yourself in, in future. So, it may be necessary to be a ‘rebel in reverse’ as it were. That takes real courage, to set your goal and stick to it. You choose your crowd. You exercise your right to choose.
Don’t lose your freedom for the sake of anyone. Real freedom, freedom to choose the right thing, the best for you.

Always bear a few things in mind while exercising your right to choose.

* Never take a decision when you are in a fit of anger or depression.
* Never take a decision when you are emotionally high.
* Why should fads or the decision of the group tie you down?
* What are you?
* What do you want tomorrow to be for you?

No matter how strong the group decision may be, you must think and make your decision. Many times it is necessary to consult before taking a decision. Go to someone whose life you admire, not necessarily the person you like most, but the person who is whole, who is one person, wherever she or he is and whatever she or he does.

* Remember that there is always tomorrow, and tomorrow is hope. Very few things are ‘written in stone’. Most of the mistakes we make can be rectified. They can be corrected. Problems have a solution, and each new day is a new start, a new chance, a New Hope. Indeed the youth are our hope you are our future.

Also remember that your parents love you unconditionally, you have their support and want the best in life for you ¨

COSTA VICTOR NAMPOKA

Mguu ulivyokatisha ndoto za kucheza soka Ulaya

DANIEL MBEGA
Dar es Salaam

NI majira ya saa 5.20 hivi asubuhi, niko hapa Ukonga-Banana nikiwania kupanda daladala la kwenda kwenye kitongoji cha Kitunda-Kibeberu, moja ya vitongoji vinavyokua kwa kasi hapa jijini Dar es Salaam.
Sijui ni umbali gani kutoka hapa, hivyo namuuliza dereva ambaye nimeketi naye pembeni yake. Ananiambia ni mwendo kama wa dakika 15 tu hivi. Nashusha pumzi kwa kujua kwamba kumbe si mbali sana kama nilivyofikiria.
Nawasili kwenye kitongoji cha Kibeberu, ambako ndiko magari yanakogeuzia, na bila kupoteza muda nampigia simu mwenyeji wangu kwamba tayari nimeshafika. Namhurumia huko aliko kama ataamua kuja kunipokea, lakini nafarijika anaponiambia kwamba nimuulize mtu yeyote hapo kituoni atanileta.
Watoto wawili wanajitolea kunipeleka nyumbani kwa mwenyeji wangu, ambaye namkuta akiwa kajilaza kwenye kochi akizungumza na rafiki zake wawili waliomtembelea. Anapenda kuketi vizuri, lakini hali haimruhusu.
“Poleni jamani kwa safari ndefu!” ndivyo anavyoanza kusema huyu mwenyeji wangu, ambaye si mwingine zaidi ya mlinzi mahiri wa timu ya soka ya Taifa, Taifa Stars, pamoja na klabu ya Simba, Costa Victor Nampoka ‘Nyumba’. Anajaribu kuuweka vyema mguu wake wa kulia ambao bado umefungwa bandeji gumu (POP) baada ya kuvunjia mazoezini takribani mwezi mmoja na nusu uliopita.
“Hakuna shaka, Dar es Salaam ni moja na hakuna sehemu unayoweza kusema ni mbali,” namjibu kumpa matumaini.
“Hapana! Pamoja na ukweli kwamba mkoa kazini, lakini naamini uamua kufunga safari mpaka kuja kuniona ni jambo kubwa sana. Mngeweza hata kuniuliza maendeleo yangu kwa njia ya simu. Sina budi kushukuru kwa kuja kunijulia hali,” anasema.
Mara anaingia dada mmoja mweupe hivi ambaye anaketi pamoja na Costa kwenye kochi moja. Costa mwenyewe anamtambulisha kwamba ndiye mkewe, Dina, ambaye wamebahatika kuzaa naye watoto wawili; Victor Costa mwenye miaka miwili na Rio Costa mwenye mwaka 1.5. Anatukaribisha.
Anapoondoka namwambia ni jambo la kawaida kuwatembelea wagonjwa, na katika suala lake yeye ni mmoja wa watu waliotoa mchango mkubwa katika timu ya taifa ya soka ambayo sasa iko katika nafasi nzuri ya kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika mwakani ikiwa tu itashinda mechi yake ya mwisho.
“Nashukuru kusikia hivyo, lakini sura zinazokuja hapa daima ni zile nilizozizowea, yaani marafiki zangu na wachezaji wenzangu wa klabu ya Simba, labda na viongozi wa Simba,” anasema kwa huzuni.
“Una maana kwamba viongozi wa timu ya taifa na hata TFF huwa hawakutembelei?” nauliza.
Anasema tangu alipoumia siku tatu kabla ya Taifa Stars kupambana na Zambia katika mechi ya kirafiki na kupelekwa Muhimbili na daktari wa timu Shecky Mngazija, hajatembelewa wala kujuliwa hali hata kwa simu na kiongozi yeyote yule wa chombo hicho cha juu cha soka nchini.
Anaongeza kwamba, ni wachezaji wenzake wa Simba ndio baadhi yao huwa wanawasiliana naye pamoja na viongozi na marafiki wa klabu ambao wameonekana kumjali vya kutosha kiasi cha kutuma gari kila siku katika mechi zote ambazo Simba ilicheza kwenye hatua ya Sita Bora ya Ligi ya Mpito hadi fainali.
“Kwa kweli viongozi wa klabu yangu wananijali sana na sina budi kuwashukuru,” anasema. Kama vile amekumbuka kitu, anasema anamshukuru pia mtu mmoja wa Benki ya NMB anayeitwa Kajura (Imani Kajura ambaye ni Meneja Masoko).
“Huyu jamaa baada ya kutoa zawadi za shilingi 500,000 kwa kila mchezaji kutokana na timu ya Taifa kushinda kule Burkina Faso, alinipigia simu kuniambia nilitakiwa kwenda kusaini fomu za akaunti. Nikamwambia sina hata pesa ya nauli na kwa jinsi ninavyoumwa nisingeweza kupanda daladala, lakini akaniambia nichukue teksi nay eye angelipa. Namshukuru sana,” anasema.
Hata hivyo, amewaasa wachezaji wengine; wa klabu na hata timu ya taifa, kwamba pindi watakapoumia na kushindwa kujuliwa hali na viongozi wao wasife moyo bali hiyo iwe changamoto kwao kufanya vizuri watakaporejea uwanjani.
“Binafsi sina kinyongo na yeyote. Naomba Mungu nipone nirejee uwanjani, ikibidi niliwakilishe taifa langu, kwa sababu natambua kwamba timu ya Taifa ni ya Watanzania wote wala si ya mtu mmoja. Naamini Watanzania milioni kadhaa wako pamoja na mimi na hata walipojua kwamba nimeumia walinitumia meseji za pole zaidi ya 3,000, hata sijui walikoipata namba yangu,” anasema.

Kuvunjika mguu
Costa anasema kwamba walikuwa kwenye mazoezi kama kawaida kwenye uwanja wa Karume, akauzuia mpira bila kumkwatua ama kukwatuliwa, kisha akaserereka.
“Ghafla nikasikia maumivu makali sana, ikabidi wajaribu kuniganga pale, lakini yalipozidi wakanikimbiza Muhimbili. Huko nikaambiwa kwamba nimevunjika mfupa mdogo wa mguu wa kulia. Sikuwa na jinsi, wakanifunga hogo (bandeji gumu – POP) na kusema kwamba nirudi baada ya wiki sita,” anasema kwa majonzi.
Anasema kwamba, baada ya kutolewa kwa bandeji hilo ndipo atakapojua kama atakuwa nje ya uwanja kwa muda gani, kwani mpaka sasa hajaanza hata kuukanyangia mguu huo.
Akasema kuvunjika mguu kumemnyima nafasi ya kuliwakilisha taifa, na zaidi kumechelewesha kutimia kwa ndoto zake kwani pengine hivi sasa angeweza kuwa Afrika Kusini kujaribu kucheza soka ya kulipwa akiwa njiani kwenda cheza Ulaya.
“Kuna wakala mmoja ambaye kwa muda mrefu sasa amekuwa akinufuatilia, yuko Afrika Kusini, na alikwenda Burkina Faso kunitazama, lakini mimi sikuwepo. Ilikuwa niende Afrika Kusini kufanya majaribio na naamini ningewea kufanikiwa,” anasema mchezaji huyo.
Anasema kwamba, alikuwa na matumaini ya kufuzu kwa sababu soka ya Afrika Kusini haina tofauti na ya huku, tena hakuwa mgeni baada ya kucheza kwa muda nchini humo miaka mitatu iliyopita.
“Wanachotuzidi kule ni promosheni, televisheni zinajitahidi sana kuonyesha mpira hata wa daraja la tatu, na hiyo inamsaidia mchezaji kutazama na kuona wapi alipokosea ili kujirekebisha, ama afanye nini kuongeza jitihada,” anasema.
Anaongeza kwamba alishindwa kuendelea kucheza huko kwa sababu klabu aliyokuwa akiichezea wakati ule ya Marlasburg (Tembas) iliyokuwa daraja la kwanza mwaka 2005 ikiwa chini ya kocha wa zamani wa Simba Trott Moloto, iliinunua klabu moja iliyokuwa ligi kuu. Ikabidi wachezaji wa timu hizo wachekechwe, na majungu ndipo yakaibuka ambapo Moloto, ambaye ndiye aliyemfanyia mpango wa kwenda huko, akamgeuka. Ikabidi afungashe virago kurejea.
Hata hivyo, anasema kwamba ndoto zake bado hazijafutika, kwani anaamini anaweza kucheza Ulaya bila matatizo yoyote, na zaidi anasema angependa siku moja avae ‘uzi’ wa Manchester United akicheza pembeni ya Rio Ferdnand ambaye uchezaji wake unamvutia kiasi cha kumwitia mwanawe mdogo jina hilo kutokana na kumhusudu.
Akizungumzia nafasi ya Taifa Stars kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika mwakani, Costa (25) ambaye ni mtoto wa nne katika familia ya watoto watano wa mzee Victor Nampoka – wawili wanawake na watatu wanaume, anasema kwamba nafasi ipo, lakini mechi ya mwisho dhidi ya Msumbiji ni ngumu sana.
“Ile mechi ni kama fainali na inabidi maandalizi ya nguvu yafanyike pengine kuliko mechi zote zilizotangulia. Msumbiji ni wazuri sana kuliko hata Burkina Faso, na ina nafasi ya kufuzu ikiwa itashinda na Senegal wakafungwa, hivyo Watanzania tusibweteke bali tujiandae vizuri,” anasema huku akisikitika kwamba anaweza kuikosa mechi hiyo pia ikiwa ataambiwa apumzike.
Akizungumzia kuhusu maendeleo ya soka, mlinzi huyo anasema kwamba hakuna kitakachoinua zaidi ya soka la vijana, na kuongeza kwamba mashindano ya Copa Coca Cola yawe chachu wa klabu na wadau mbalimbali kuanza kuibua vipaji.
“Kule Brazil tulikokwenda kuna taasisi ya soka ya watoto wadogo. Watoto wanatoka nchi mbalimbali kwenda kufundishwa mpira, na wazazi wao wanalipia wastani wa dola 1,500 kwa mwezi ili watoto wao wajue mpira. Tusione wenzetu wamepiga hatua tukadhani kwamba ni miujiza, wamewekeza.
“Watanzania wanapaswa kuunga mkono juhudi za maendeleo ya soka ya vijana, kuanzia kwa wazazi, ambao wanapaswa kuwapa ‘sapoti’ watoto wao ikiwa ni pamoja na kuwapatia vifaa vya michezo na nauli ya kwenda mazoezini,” anaongeza.
Costa aliyemaliza elimu ya msingi mwaka 1994 Kinondoni Hananasif, jijini Dar es Salaam na kuungana na maelfu ya watoto ambao hawakufanikiwa kuchaguliwa kujiunga na sekondari, amewashauri wachezaji kuachana na anasa na kwamba wawe na malengo kama kweli wanataka kupiga hatua katika mchezo huo.
“Sijafanikiwa sana, lakini niseme ukweli kwamba nimejiepusha na mambo mengi. Sivuti sigara wala bangi, halafu niliacha kitambo kunywa pombe, tena basi nilikuwa nikinywa bia mbili ama tatu tu, lakini sasa sitaki kabisa nahitaji kukazana kwenye mpira ambao pekee ndio mwokozi wangu katika maisha,” anamalizia.

Wasifu:
Jina: Costa Victor Nampoka
Kuzaliwa: Oktoba 11, 1982, Dar es Salaam.
Umri: 25

Klabu za awali:
Five Star Kinondoni, Mkunguni FC Ilala, Eleven FC Buguruni, Saddam FC na International FC za Kinondoni.
Taifa Jang’ombe – Zanzibar (1998 – 1999)
Forodha Zanzibar (2000 – 2001)
Mtibwa Sugar (2002)
Simba (2003 – 2004)
Marlsburg – Afrika Kusini (2005)
Simba (2006 – mpaka sasa).