Friday, August 20, 2010

Watanzania ‘wana imani’ na Dk. Slaa
*Anauzika, anachagulika na mzalendo wa kweli
Na Clement Magembe
DK.WILLIBROD Peter Slaa ,Katibu Mkuu wa CHADEMA ambaye amependekezwa na chama hicho kuwania nafasi ya urais anatajwa kuwa ni mwiba mkali kwa mgombea wa nafasi hiyo kwa tiketi ya CCM, Rais Jakaya Kikwete.
Dk. Slaa ni jina ambalo limekuwa likisikika sana katika jamii ya Watanzania kutokana na kuonekana kama shujaa aliyekuwa na utayari wa kuthubutu kupigana vita dhidi ya “wakoloni wazawa” au mafisadi kama wanavyofahamika sasa, waliojitokeza kwa ajili ya kudhulumu rasilimali zilizopo nchini kwa maslahi yao binafsi na watu wanaoingizwa nchini kwa kivuli cha uwekezaji.
Watanzania wengi wanathibitisha kuwa ni kiongozi safi na bora, shujaa, mkakamavu na mkemea hila na mienendo mibaya ya watu walioko madarakani waliozoea kuwayumbisha Wananchi tangu kupatikana kwa uhuru wa taifa hili na pia kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kuigawa jamii baina ya matajiri na masikini ambao ndio wengi wanaopoteza maisha baada ya kupokea ahadi hewa kutoka kwa wagombea urais, ubunge na udiwani.
Jina la Dk.Slaa sio geni miongoni mwa Watanzania wengi kutokana na mchango wake kufichua “ufisadi” uliofanyika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na maeneo mengine na kuithibitishia jamii ya Watanzania kuwa wafanyabiashara walioamua kufanyabiashara na chama tawala na baadhi ya viongozi waliokosa uaminifu kwa kulitumikia taifa kwa mujibu wa ‘mashairi’ ya ilani zao walizozinadi wakati wa kuomba ajira kwa wapiga kura.
Sakata la wizi wa fedha za EPA ndani ya BoT hili ndilo limefanya jina lake liwe miongoni mwa majina maarufu sio tu kutoka kambi ya upinzani bali katika anga za wanasiasa nchini Tanzania.
Dk.Slaa alizaliwa katika kijiji cha Kwermusl, Wilaya ya Mbulu Oktoba 10, mwaka 1948 na kupata taaluma ndani na nje ya Nchi hadi kufikia hadhi ya Udaktari wa Falsafa na kuamua kuingia katika uwanja wa siasa mwaka 1995.
Awali alishiriki shughuli mbalimbali za uongozi akiwa katibu wa TANU Youth League Seminari ya Kipalapala na kufungua matawi mengi ya TANU wakati huo, Katibu wa Shina la CCM, Tawi la Mambo ya Nje, Rome mwaka 1980.
Aliamua kugombea ubunge baada ya Wazee wa Karatu kumfuata akiwa jijini Dar es Salaam wakati wa uchaguzi mkuu uliovirikisha vyama vingi vya siasa wa vyama huku vilivyokuwa na nguvu kubwa ikiwa ni pamoja na CCM, Chadema, NCCR-Mageuzi na CUF.
DK.Slaa aliingia kwenye uwanja wa kisiasa kupitia CCM ambacho alikichagua kutoka awali na kushinda kura za maoni lakini jina lake liliondolewa kwa mizengwe kwa sababu yeye “hakuwa mwenzao” na kwamba alifahamu baadae kuwa alipotea njia kutokana na hali ya ufisadi iliyojitokeza.
Pamoja na hayo anaeleza kuwa hakujutia kabisa hali hiyo na kuamua kujiunga na Chadema na kufanikiwa kupata nafasi hiyo na kuwatumikia Wananchi wa Karatu kama alivyowaahidi.
Slaa alikuwa Padre wa Kanisa Katoliki na kushika nafasi za juu za uongozi ndani ya Kanisa hilo kuanzia jimboni kwake akiwa Makamu wa Askofu, Mkurugenzi wa Maendeleo na Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu (TEC) 1985 hadi 1991 na kuamua kuachana na Upadre bila kushinikizwa na yeyote, wala kufukuzwa, wala hata kupewa onyo, wala kuwa na ugomvi wa aina yeyote na Kanisa Katoliki na mshiriki wa shughuli mbalimbali za Kanisa.
Achilia mbali historia aliyojingea kwa kipindi chote alichokuwa akishikilia nafasi ya ubunge huku akiiadhibu serikali ya CCM kwa kufichua kila namna uovu uliokuwa umesitirika kwa kipindi kirefu huku chama hicho kikigeuzwa kama pango la wanyang’anyi wasiojali wala kuthamini haki za Wananchi wa kawaida.
Dk. Slaa ambaye anakuwa silaha kali ya kanisa Katoliki lenye idadi kubwa ya wafuasi nchini anaelezwa kuwa ni chaguo la kanisa hilo ambalo hivi karibuni kwa nyakati tofauti litoa waraka wake unaotaka kuchaguliwa kwa viongozi wa nchi walio chini ya dhehebu hilo watakaotekeleza wajibu wao wa kuitumikia jamii baada ya umaarufu wa CCM kuonekana kuyumba kutokana na baadhi ya wanachama na wafadhili wake kuonekana ni watu ovyo na watuhumiwa wa ufisadi.
Kuteuliwa kwa Dk.Slaa kuwania nafasi ya urais kwa tiketi ya Chadema hakuungwi mkono na kanisa Katoliki tu bali wananchi wa kada mbalimbali wapenda mabadiliko na wengi wao wanatajwa kuwa Wafanyakazi wa serikali ambao rais Kikwete aliwaeleza kuwa hazihitaji kura zao baada ya kutishia mgomo ili kushinikiza nyongeza ya mishahara yao na kuwakataa viongozi wa serikali kuwa wageni rasmi katika maadhimisho ya Siku kuu ya Wafanyakazi (Mei Mosi) mwaka huu.
Wachunguzi wa masuala ya kisiasa wanaeleza kuwa wanachotazamia ni mabadiliko makubwa ya kiutawala nap engine kuutokomeza utawala dhaifu ambao umekuwa chanzo cha umasikini kwa Watanzania baada kuingiliwa na kundi la wafanyabiashara matapeli waliojiingiza kufanya biashara na Serikali kwa mgongo wa ufadhili wa CCM.
Kutokana na hali ilivyo sasa huku migogoro baina ya Wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, Waislamu wanaodai ahadi ya Mahakama ya Kadhi na OIC na mengine ushindani mkubwa utaibuka katika uchaguzi mkuu ikiwa tofauti kabisa na chaguzi zilizopita.
Hakuna mtetezi tena kwa CCM aliye na sauti ya kuonya ili kukinusuru chama hicho ama kutuliza hasira za Wananchi wanaoishi maisha bora ya kufikirika sambamba na kejeri za mafanikio ya misongamano ya magari katika barabara za Jiji la Dar es Salaam.
Ufisadi, rushwa na madudu mengine yanayoonyeshwa na waliojitokeza kuwania nafasi za ubunge na udiwani kwa tiketi ya CCM ni fimbo nyingine ya wananchi kutaka mabadiliko ya Uongozi, Katiba, Tume Huru ya Uchaguzi baada ya kwa kuichagua kambi ya upinzani na lengo kubwa likiwa ni kunufaika na rasilimali za taifa hili ambazo zinawanufaisha watu wachache na wageni huku maelfu wakipoteza maisha kwa kukosa huduma za afya.
Lakini jambo jingine ambalo linakuwa ni mwiba kwa CCM na kikomo cha utawala wake ni kile kinachoelezwa kuwa ni kukorofishana na Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Zachary Kakobe, ambaye alikuwa mtetezi mkubwa wa serikali ya awamu ya nne baada ya Maaskofu wa Katoliki na Waumini wa dini ya Kiislamu kuitisha serikali kwa nyaraka nzito zilizoonesha kuuchukia utawala wake.
“Sasa hawana mtetezi kabisa na kila mmoja anafanya jitihada zake mwenyewe ili kuingia madarakani au kuanguka, utawala wa CCM umefitinika na hakuna unafuu mamilioni ya Wananchi wanyonge watamuunga mkono Dk. Slaa ili kuliletea maendeleo ya kweli taifa hili”, alieleza Richard Conrad aliyejitambulisha kuwa ni mwanachama wa CCM mpenda mabadiliko na mkazi wa Kimara Bucha Jijini Dar es Salaam.
Anasema kuwa CCM haina mtetezi kwa kuwa watu wamechoka na ufisadi huku watuhumiwa wakikingiwa kifua kwa kufunguliwa kesi zinazoendeshwa kwa mfumo wa filamu na michezo ya mazingaombwe.
Anasema kuwa uongozi wa kununua kwa sasa utafikia kikomo baada ya wanyonge kutafuta ukombozi baada ya kilio cha muda mrefu na uziwi wa viongozi wa serikali ambao hawataki kusikia wala kuelezwa lolote lile licha ya kutoa ahadi za kilaghai.
Chadema inajulikana wazi kwa misimamo yake katika maswali mbalimbali ikiwemo kushindwa kwa CCM kupiga vita rushwa, taifa kupoteza mwelekeo katika mambo mbalimbali huku Serikali ikigeuka kiziwi na kujipongeza na miradi ya MMEM na MMES, ambayo kimsingi si sera yao ikiwa imetokana na maamuzi ya Kimataifa yaliyofanyika Jomtien, Thailand, mwaka 1990.
Uchafu ulioambatana na kuchota fedha BoT, Tangold, Meremeta kupitia DEEP GREEN,kuingiza serikali katika mkataba wa kitapeli wa kampuni ya kufua umeme ya RICHMOND na tuhuma zingine zilizoibuliwa na kambi ya upinzania umekitia kiwewe chama hicho ambacho sasa kimebakiwa na propaganda za kisiasa zikiambatana na ilani zisizotekelezeka jambo linaloacha maswali juu ya usalama wa rasilimali za umma.
SOURCE: DIRA YA MTANZANIA.

No comments:

JUST ANOTHER THOUGHT

JUST ANOTHER THOUGHT

A person asked God, “What surprises you most about mankind?”

And God answered,
“That they loose their Health to make money and they loose their money to restore their Health.

That by thinking anxiously about the future, they forget the present, such that they live neither for the present nor the future.

That they live as if they will never die and they die as if they had never lived.….”

BECAUSE I'M A MAN...

Because I’m a man, when one of our appliances stops working I will insist on taking it apart, despite evidence that this will just cost me twice as much once the repair person gets here and has to put it back together.

Because I’m a man, I don’t think we’re all that lost, and no, I don’t think we should stop and ask someone. Why would you listen to a complete stranger I mean, how the hell could he know where we’re going?

Because I’m a man, there is no need to ask me what I’m thinking about. The answer is always either sex or football, though I have to make up something else when you ask, so don’t.

Because I’m a man, I do not want to visit your mother, come visit us, or talk to her when she calls, or think about her any more than I have to. Whatever you got her for mother’s day is okay, I don’t need to see it. And don’t forget to pick up something for my mommy, too!

Because I’m a man, I am capable of announcing, “one more beer and I really have to go”, and mean it every single time I say it, even when it gets to the point that the one bar closes and my buddies and I have to go hunt down another. I will find it increasingly hilarious to have my pals call you to tell you I’ll be home soon, and no, I don’t understand why you threw all my clothes into the front yard. Like, what’s the connection?

Because I’m a man, you don’t have to ask me if I liked the movie. Chances are, if you’re crying at the end of it, I didn’t.

Because I’m a man, yes, I have to turn up the radio when Bruce Springsteen or The Doors comes on, and then, yes, I have to tell you every single time about how Bruce had his picture on the cover of Time and Newsweek the same day, or how Jim Morrison is buried in Paris and everyone visits his grave. Please do not behave as if you do not find this fascinating.

Because I’m a man, I think what you’re wearing is fine. I thought what you were wearing five minutes ago was fine, too. Either pair of shoes is fine. With the belt or without it looks fine. Your hair is fine. You look fine. Can we just go now?

Because I’m a man and this is, after all, the 90’s, I will share equally in the housework. You just do the laundry, the cooking, the gardening, the cleaning, and the dishes. I’ll do the rest.

A SIMPLE GUIDE TO LIFE

1. Follow your dream! Unless it’s the one where you’re at work in your underwear during a fire drill.

2. Always take time to stop and smell the roses and sooner or later, you’ll inhale a bee.

3. Do not walk behind me, for I may not lead. Do not walk ahead of me, for I may not follow. Do not walk beside me, either. Just leave me alone.

4. If you don’t like my driving, don’t call anyone. Just take another road. That’s why the highway department made so many of them.

5. If a motorist cuts you off, just turn the other cheek. Nothing gets the message across like a good mooning.

6. When I’m feeling down, I like to whistle. It makes the neighbor’s dog run to the end of his chain and gag himself.

7. It’s always darkest before dawn. So if you’re going to steal the neighbor’s newspaper, that’s the time to do it.

8. A handy telephone tip: Keep a small chalkboard near the phone. That way, when a salesman calls, you can hold the receiver up to it and run your fingernails across it until he hangs up.

9. Each day I try to enjoy something from each of the four groups: the bonbon group, that salty-snack group, the caffeine group and the “What ever-it-is-the-tinfoil-in-the-back-of-the-fridge”.

10. Into every life some rain must fall. Unusually when your car windows are down.

11. Just remember: You gotta break some eggs to make a real mess on the neighbor’s car!

12. When you find yourself getting irritated with someone, try to remember that all men are brothers and just give them a noogie.

13. This morning I woke up to the unmistakable scent of pigs in a blanket. That’s the price you pay for letting the relatives stay over.

14. It’s a small world. So you gotta use your elbows a lot.

15. Keep your nose to the grindstone and your shoulder to the wheel. It’s a lot cheaper than plastic surgery.

16. This land is your land. This land is my land. So stay in your land.

17. Love is like a roller coaster: When it’s good you don’t want to get off, and when it isn’t, you can’t wait to throw up.

DEDICATION TO YOUNG PEOPLE

Youth is a time of hope. Also of uncertainty. But for a person who is young and healthy, uncertainty just means a challenge. It is important to be positive. First of all about yourself. But also about your family and your people. As a unique person and each human being are unique, you have enormous potential. Because you have so much potential, people may sometimes feel negatively challenged by that potential and try to undermine it.

You have to fight for your right to make your place in society. To do that you have to use all the chances given you now to be a positive element in whatever situation you find yourself in, in future. So, it may be necessary to be a ‘rebel in reverse’ as it were. That takes real courage, to set your goal and stick to it. You choose your crowd. You exercise your right to choose.
Don’t lose your freedom for the sake of anyone. Real freedom, freedom to choose the right thing, the best for you.

Always bear a few things in mind while exercising your right to choose.

* Never take a decision when you are in a fit of anger or depression.
* Never take a decision when you are emotionally high.
* Why should fads or the decision of the group tie you down?
* What are you?
* What do you want tomorrow to be for you?

No matter how strong the group decision may be, you must think and make your decision. Many times it is necessary to consult before taking a decision. Go to someone whose life you admire, not necessarily the person you like most, but the person who is whole, who is one person, wherever she or he is and whatever she or he does.

* Remember that there is always tomorrow, and tomorrow is hope. Very few things are ‘written in stone’. Most of the mistakes we make can be rectified. They can be corrected. Problems have a solution, and each new day is a new start, a new chance, a New Hope. Indeed the youth are our hope you are our future.

Also remember that your parents love you unconditionally, you have their support and want the best in life for you ¨

COSTA VICTOR NAMPOKA

Mguu ulivyokatisha ndoto za kucheza soka Ulaya

DANIEL MBEGA
Dar es Salaam

NI majira ya saa 5.20 hivi asubuhi, niko hapa Ukonga-Banana nikiwania kupanda daladala la kwenda kwenye kitongoji cha Kitunda-Kibeberu, moja ya vitongoji vinavyokua kwa kasi hapa jijini Dar es Salaam.
Sijui ni umbali gani kutoka hapa, hivyo namuuliza dereva ambaye nimeketi naye pembeni yake. Ananiambia ni mwendo kama wa dakika 15 tu hivi. Nashusha pumzi kwa kujua kwamba kumbe si mbali sana kama nilivyofikiria.
Nawasili kwenye kitongoji cha Kibeberu, ambako ndiko magari yanakogeuzia, na bila kupoteza muda nampigia simu mwenyeji wangu kwamba tayari nimeshafika. Namhurumia huko aliko kama ataamua kuja kunipokea, lakini nafarijika anaponiambia kwamba nimuulize mtu yeyote hapo kituoni atanileta.
Watoto wawili wanajitolea kunipeleka nyumbani kwa mwenyeji wangu, ambaye namkuta akiwa kajilaza kwenye kochi akizungumza na rafiki zake wawili waliomtembelea. Anapenda kuketi vizuri, lakini hali haimruhusu.
“Poleni jamani kwa safari ndefu!” ndivyo anavyoanza kusema huyu mwenyeji wangu, ambaye si mwingine zaidi ya mlinzi mahiri wa timu ya soka ya Taifa, Taifa Stars, pamoja na klabu ya Simba, Costa Victor Nampoka ‘Nyumba’. Anajaribu kuuweka vyema mguu wake wa kulia ambao bado umefungwa bandeji gumu (POP) baada ya kuvunjia mazoezini takribani mwezi mmoja na nusu uliopita.
“Hakuna shaka, Dar es Salaam ni moja na hakuna sehemu unayoweza kusema ni mbali,” namjibu kumpa matumaini.
“Hapana! Pamoja na ukweli kwamba mkoa kazini, lakini naamini uamua kufunga safari mpaka kuja kuniona ni jambo kubwa sana. Mngeweza hata kuniuliza maendeleo yangu kwa njia ya simu. Sina budi kushukuru kwa kuja kunijulia hali,” anasema.
Mara anaingia dada mmoja mweupe hivi ambaye anaketi pamoja na Costa kwenye kochi moja. Costa mwenyewe anamtambulisha kwamba ndiye mkewe, Dina, ambaye wamebahatika kuzaa naye watoto wawili; Victor Costa mwenye miaka miwili na Rio Costa mwenye mwaka 1.5. Anatukaribisha.
Anapoondoka namwambia ni jambo la kawaida kuwatembelea wagonjwa, na katika suala lake yeye ni mmoja wa watu waliotoa mchango mkubwa katika timu ya taifa ya soka ambayo sasa iko katika nafasi nzuri ya kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika mwakani ikiwa tu itashinda mechi yake ya mwisho.
“Nashukuru kusikia hivyo, lakini sura zinazokuja hapa daima ni zile nilizozizowea, yaani marafiki zangu na wachezaji wenzangu wa klabu ya Simba, labda na viongozi wa Simba,” anasema kwa huzuni.
“Una maana kwamba viongozi wa timu ya taifa na hata TFF huwa hawakutembelei?” nauliza.
Anasema tangu alipoumia siku tatu kabla ya Taifa Stars kupambana na Zambia katika mechi ya kirafiki na kupelekwa Muhimbili na daktari wa timu Shecky Mngazija, hajatembelewa wala kujuliwa hali hata kwa simu na kiongozi yeyote yule wa chombo hicho cha juu cha soka nchini.
Anaongeza kwamba, ni wachezaji wenzake wa Simba ndio baadhi yao huwa wanawasiliana naye pamoja na viongozi na marafiki wa klabu ambao wameonekana kumjali vya kutosha kiasi cha kutuma gari kila siku katika mechi zote ambazo Simba ilicheza kwenye hatua ya Sita Bora ya Ligi ya Mpito hadi fainali.
“Kwa kweli viongozi wa klabu yangu wananijali sana na sina budi kuwashukuru,” anasema. Kama vile amekumbuka kitu, anasema anamshukuru pia mtu mmoja wa Benki ya NMB anayeitwa Kajura (Imani Kajura ambaye ni Meneja Masoko).
“Huyu jamaa baada ya kutoa zawadi za shilingi 500,000 kwa kila mchezaji kutokana na timu ya Taifa kushinda kule Burkina Faso, alinipigia simu kuniambia nilitakiwa kwenda kusaini fomu za akaunti. Nikamwambia sina hata pesa ya nauli na kwa jinsi ninavyoumwa nisingeweza kupanda daladala, lakini akaniambia nichukue teksi nay eye angelipa. Namshukuru sana,” anasema.
Hata hivyo, amewaasa wachezaji wengine; wa klabu na hata timu ya taifa, kwamba pindi watakapoumia na kushindwa kujuliwa hali na viongozi wao wasife moyo bali hiyo iwe changamoto kwao kufanya vizuri watakaporejea uwanjani.
“Binafsi sina kinyongo na yeyote. Naomba Mungu nipone nirejee uwanjani, ikibidi niliwakilishe taifa langu, kwa sababu natambua kwamba timu ya Taifa ni ya Watanzania wote wala si ya mtu mmoja. Naamini Watanzania milioni kadhaa wako pamoja na mimi na hata walipojua kwamba nimeumia walinitumia meseji za pole zaidi ya 3,000, hata sijui walikoipata namba yangu,” anasema.

Kuvunjika mguu
Costa anasema kwamba walikuwa kwenye mazoezi kama kawaida kwenye uwanja wa Karume, akauzuia mpira bila kumkwatua ama kukwatuliwa, kisha akaserereka.
“Ghafla nikasikia maumivu makali sana, ikabidi wajaribu kuniganga pale, lakini yalipozidi wakanikimbiza Muhimbili. Huko nikaambiwa kwamba nimevunjika mfupa mdogo wa mguu wa kulia. Sikuwa na jinsi, wakanifunga hogo (bandeji gumu – POP) na kusema kwamba nirudi baada ya wiki sita,” anasema kwa majonzi.
Anasema kwamba, baada ya kutolewa kwa bandeji hilo ndipo atakapojua kama atakuwa nje ya uwanja kwa muda gani, kwani mpaka sasa hajaanza hata kuukanyangia mguu huo.
Akasema kuvunjika mguu kumemnyima nafasi ya kuliwakilisha taifa, na zaidi kumechelewesha kutimia kwa ndoto zake kwani pengine hivi sasa angeweza kuwa Afrika Kusini kujaribu kucheza soka ya kulipwa akiwa njiani kwenda cheza Ulaya.
“Kuna wakala mmoja ambaye kwa muda mrefu sasa amekuwa akinufuatilia, yuko Afrika Kusini, na alikwenda Burkina Faso kunitazama, lakini mimi sikuwepo. Ilikuwa niende Afrika Kusini kufanya majaribio na naamini ningewea kufanikiwa,” anasema mchezaji huyo.
Anasema kwamba, alikuwa na matumaini ya kufuzu kwa sababu soka ya Afrika Kusini haina tofauti na ya huku, tena hakuwa mgeni baada ya kucheza kwa muda nchini humo miaka mitatu iliyopita.
“Wanachotuzidi kule ni promosheni, televisheni zinajitahidi sana kuonyesha mpira hata wa daraja la tatu, na hiyo inamsaidia mchezaji kutazama na kuona wapi alipokosea ili kujirekebisha, ama afanye nini kuongeza jitihada,” anasema.
Anaongeza kwamba alishindwa kuendelea kucheza huko kwa sababu klabu aliyokuwa akiichezea wakati ule ya Marlasburg (Tembas) iliyokuwa daraja la kwanza mwaka 2005 ikiwa chini ya kocha wa zamani wa Simba Trott Moloto, iliinunua klabu moja iliyokuwa ligi kuu. Ikabidi wachezaji wa timu hizo wachekechwe, na majungu ndipo yakaibuka ambapo Moloto, ambaye ndiye aliyemfanyia mpango wa kwenda huko, akamgeuka. Ikabidi afungashe virago kurejea.
Hata hivyo, anasema kwamba ndoto zake bado hazijafutika, kwani anaamini anaweza kucheza Ulaya bila matatizo yoyote, na zaidi anasema angependa siku moja avae ‘uzi’ wa Manchester United akicheza pembeni ya Rio Ferdnand ambaye uchezaji wake unamvutia kiasi cha kumwitia mwanawe mdogo jina hilo kutokana na kumhusudu.
Akizungumzia nafasi ya Taifa Stars kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika mwakani, Costa (25) ambaye ni mtoto wa nne katika familia ya watoto watano wa mzee Victor Nampoka – wawili wanawake na watatu wanaume, anasema kwamba nafasi ipo, lakini mechi ya mwisho dhidi ya Msumbiji ni ngumu sana.
“Ile mechi ni kama fainali na inabidi maandalizi ya nguvu yafanyike pengine kuliko mechi zote zilizotangulia. Msumbiji ni wazuri sana kuliko hata Burkina Faso, na ina nafasi ya kufuzu ikiwa itashinda na Senegal wakafungwa, hivyo Watanzania tusibweteke bali tujiandae vizuri,” anasema huku akisikitika kwamba anaweza kuikosa mechi hiyo pia ikiwa ataambiwa apumzike.
Akizungumzia kuhusu maendeleo ya soka, mlinzi huyo anasema kwamba hakuna kitakachoinua zaidi ya soka la vijana, na kuongeza kwamba mashindano ya Copa Coca Cola yawe chachu wa klabu na wadau mbalimbali kuanza kuibua vipaji.
“Kule Brazil tulikokwenda kuna taasisi ya soka ya watoto wadogo. Watoto wanatoka nchi mbalimbali kwenda kufundishwa mpira, na wazazi wao wanalipia wastani wa dola 1,500 kwa mwezi ili watoto wao wajue mpira. Tusione wenzetu wamepiga hatua tukadhani kwamba ni miujiza, wamewekeza.
“Watanzania wanapaswa kuunga mkono juhudi za maendeleo ya soka ya vijana, kuanzia kwa wazazi, ambao wanapaswa kuwapa ‘sapoti’ watoto wao ikiwa ni pamoja na kuwapatia vifaa vya michezo na nauli ya kwenda mazoezini,” anaongeza.
Costa aliyemaliza elimu ya msingi mwaka 1994 Kinondoni Hananasif, jijini Dar es Salaam na kuungana na maelfu ya watoto ambao hawakufanikiwa kuchaguliwa kujiunga na sekondari, amewashauri wachezaji kuachana na anasa na kwamba wawe na malengo kama kweli wanataka kupiga hatua katika mchezo huo.
“Sijafanikiwa sana, lakini niseme ukweli kwamba nimejiepusha na mambo mengi. Sivuti sigara wala bangi, halafu niliacha kitambo kunywa pombe, tena basi nilikuwa nikinywa bia mbili ama tatu tu, lakini sasa sitaki kabisa nahitaji kukazana kwenye mpira ambao pekee ndio mwokozi wangu katika maisha,” anamalizia.

Wasifu:
Jina: Costa Victor Nampoka
Kuzaliwa: Oktoba 11, 1982, Dar es Salaam.
Umri: 25

Klabu za awali:
Five Star Kinondoni, Mkunguni FC Ilala, Eleven FC Buguruni, Saddam FC na International FC za Kinondoni.
Taifa Jang’ombe – Zanzibar (1998 – 1999)
Forodha Zanzibar (2000 – 2001)
Mtibwa Sugar (2002)
Simba (2003 – 2004)
Marlsburg – Afrika Kusini (2005)
Simba (2006 – mpaka sasa).