Friday, August 20, 2010

Tuwapime, tuwachambue kama wanafaa kupewa dhamana ya uongozi

* Tujiulize, ni nani aliyewapa hatimiliki ya majimbo

Na Daniel Mbega

PEPO za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 zimezidi kuvuma kila kona ya nchi hivi sasa huku tukishuhudia vikumbo na tambo mbalimbali miongoni mwa wale wanaotaka kuomba ridhaa yetu ili tuwaongoze.
Wapo ambao tayari wako madarakani, wakifanya kila linalowezekana kuendelea kubaki kwa gharama yoyote ile ili waendelee kufaidi keki ambayo wananchi wa kawaida tunaendelea kuambulia harufu tu. Lakini pia wapo ambao wanataka kuomba ridhaa kwa mara ya kwanza, ili nao wakafaidi hayo ambayo wenzao wanayapata sasa.
Katika mchakato huo, wapo pia waliopata kushika nyadhifa mbalimbali, hasa za Ubunge na Udiwani, ambao kwa sababu mbalimbali walipigwa kumbo na hawa waliopo madarakani kwa sasa, na katika kipindi ambacho wamekuwa nje wamejaribu kutafakari makosa yao na kuwasoma wapinzani wao ili wakiingia tena wasifanye makosa.
Chama cha Mapinduzi (CCM) ndicho kinachoonekana kuwa na ushindani mkubwa, kutokana na ukweli kwamba ndicho chama tawala na kina wabunge wengi kwa sasa, na ndani yake wapo wanachama wanaotaka kuwanyang’anya wenzao nafasi ya uongozi wa wananchi.
Kura za maoni ndani ya CCM zitaanza kupigwa kuanzia Agosti 10, 2010, lakini inaonyesha bayana kwamba upinzani mkali unatarajiwa kuwepo, hasa ikizingatiwa kwamba dalili zilikwishajionyesha Novemba 6, 2007 baada ya mawaziri kadhaa na wabunge kupigwa mwereka katika nafasi za uwakilishi wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya chama hicho.
Manaibu waziri watano ni miongoni mwa waliokosa nafasi katika uwakilishi wa Viti 20 NEC nao ni pamoja na Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Dk. David Mathayo, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mshariki Dk. Diodorus Kamala na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja.
Wengine ni Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mwantumu Mahiza na aliyekuwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Ritha Mlaki aliyegombea nafasi hiyo kupitia kundi la Wanawake.
Pia wapo manaibu waziri watatu wa SMZ waliotupwa chini ambao ni Jabir Makame Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Khatib Suleiman ambaye ni Naibu Waziri Kilimo, Mifugo na Mazingira na Dk. Mwinyi Haji Makame, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais.
Katika nafasi za kundi la Wanawake Tanzania Bara kuna Mbunge wa zamani wa Afrika Mashariki na sasa Mbunge Beatrice Shelukindo. Pia yupo Mbunge Tatu Ntimizi na Katibu Mkuu mstaafu wa UWT Halima Mamuya.
Katika kundi la Wazazi Tanzania Bara, hapa kulikuwa na wagombea wengi ambao ni wabunge. Katika kundi hili kuna jina moja tu la aliyeshinda ambaye si mbunge, Nondo Mohamed. Lakini pia Danhi Makanga, Ruth Msafiri, Thomas Ngawaiya na Tambwe Hiza walipoteza katika kundi hili. Ngawaiya na Hiza walitoka upinzani na walitarajiwa kupewa ‘kura za huruma’ jambo ambalo halikufanyika.
Wengine ni pamoja na wabunge Margareth Agness Mkanga, Zuhura Mikidadi na mhamasishaji wa tenzi wa CCM, Salim Shomvi Tambalizeni, Naibu Meya wa Ilala Mustafa Yakub, Mkuu wa Mkoa wa Mara (sasa yuko Arusha) Isidore Shirima na Mkuu wa Wilaya Frank Uhahula walikosa nafasi hizo.
Wanasiasa wengine maarufu waliokosa nafasi baada ya kupata kura chache ni Wilson Masilingi, Brigedia Jenerali mstaafu Hassan Ngwilizi, Tarimba Abbas, Filbert Bayi, Enock Chambiri, Christopher Gachuma, Charles Kagonji, Lucas Kisasa, Pascal Mabiti, Dk. James Msekela, Profesa Idrisa Mtulia, Abeid Mwinyimsa na Job Ndugai. Wengine ni waandishi wa habari Jacqueline Liana, Jane Mihanji, Novatus Makunga na Shyrose Banji.
Kwa hiyo utaona kuwa kutokana na yaliyojitokeza mwaka 2007, wale walioko madarakani wanahofia yasije yakatokea tena kwenye Ubunge, hatua ambayo inawafanya wale walio madarakani wafanye kila liwezekanalo kutetea vitumbua vyao visiingie mchanga. Lakini hiyo ndiyo siasa.

Umiliki wa majimbo…
“Kuna watu wanataka kuninyang’anya jimbo langu!” “Atakayetia mguu jimboni kwangu atakiona!” “Nimefanya mambo mengi, sasa waniachie jimbo langu niliendeleze!” hizi ni kauli nyingi zilizozoeleka kuonekana kwenye vyombo vya habari, hasa katika siku za karibuni.
Kauli hizi zimekuwa zikitolewa na wale walioko madarakani kwa sasa ambao wanahisi kwamba wanaoonyesha nia ya kutaka kugombea wanawanyang’anya ‘majimbo yao’.
Kwamba inakuwaje mbunge alalamike ati kuna watu wananyemelea jimbo lake, ndilo swali ambalo limekuwa likiwatatiza wachambuzi wengi wa masuala ya siasa na demokrasia! Tangu lili jimbo likawa chini ya hatimiliki ya mtu mmoja?
Kwa mujibu wa taratibu, kanuni na sheria za uchaguzi mtu anapopata ubunge huwa anadumu kwa miaka mitano kisha uchaguzi unapowadia wananchi watapima na kuamua wamrudishe au wamuondoshe ili waweke mtu mwingine atakayewahudumia vema katika suala zima la maendeleo. Wananchi wenyewe ndio wenye mamlaka ya kumchagua ama kumkataa mgombea, lakini sasa watamchagua vipi mtu ikiwa mbunge wa sasa anang'ang'ania na kukataa ushindani?
Kwa zaidi ya mwaka sasa wabunge kadhaa, wakiwemo Dk. Harrison Mwakyembe (Kyela – CCM), Aloyce Kimaro (Vunjo – CCM), Christopher Olonyoike ole-Sendeka (Simanjiro), James Lembeli (Kahama - CCM), Anne Kilango Malecela (Same Mashariki), Dk. Zainab Gama (Kibaha Mjini), Kapteni mstaafu John Chiligati (Manyoni Mashariki), Wilson Masilingi (Muleba Kusini), na wengineo wamekuwa wakilalamika ‘kuhujumiwa’ na wale wanaopita kutangaza nia.
“Wapo watu wanaojipitisha pitisha kule jimboni kwangu, nawaonya kabisa waache, maana nitawapiga mwereka wa hali ya juu,” alipata kukaririwa akisema Mbunge wa Mtera, John Samuel Malecela, akiwaonya watu walioonyesha nia ya kugombea jimboni humo.
Ukiacha Mzee Malecela, wabunge wengine kama mkewe Anne Kilango, Dk. Mwakyembe, James Lembeli, Aloyce Kimaro, Lucas Selelii, Ole Sendeka na wenzao wamekuwa wakipiga kelele kwamba kuna watu wametumwa ama kupandikizwa na watuhumiwa wa ufisadi kuwachafua majimboni kwao ili wapoteze ubunge.
‘Majeruhi’ hao wanasema kwamba, kundi la mafisadi limemwaga fedha nyingi kwenye majimbo yao kuhakikisha kwamba wanaanguka katika kinyang’anyiro cha uchaguzi wa mwaka huu.
Wanaotajwa kuhusika na njama hizo ni Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa na Mbunge wa Igunga Rostam Aziz, ambao wanadaiwa kwamba wamewaweka watu wao washindane na wale wabunge waliokuwa mstari wa mbele kuzungumzia sakata la kampuni ya Richmond Development LLC.
Kilio hicho cha wabunge hao kimevuka mpaka kwa sasa, ambapo yeyote anayejitokeza kutaka kugombea anatajwa kuwa katumwa na ama Lowassa au Rostam kumnyang’anya ‘jimbo lake’.Inafahamika vyema kwamba siasa inatumia hila nyingi, na hili wanasiasa wanalitambua fika.
Lakini kinachotia shaka ni kwamba, kwa nini kila anayejitokeza hata kwa dhamira yake binafsi awe katumwa? Hivi ni lini basi ambapo Lowassa na Rostam watachagua watu wa kuwaunga mkono badala ya kutuma?
Wapembuzi wa masuala ya siasa wanahisi kwamba, hii inaweza kuwa ni mbinu nyingine ya wanasiasa hawa wapambanaji wa ufisadi kutaka ‘huruma’ ya wapiga kura wawachague kwa kisingizio wanaonewa ili wasirudi Bungeni.
Jambo moja wanalolisahau ni kwamba, yawezekana wao wamejisahau kutekeleza ahadi zao kwa wananchi na sasa wamegeuziwa kisogo, hivyo wanakimbia vivuli vyao. Wachambuzi wa masuala ya siasa wanasema, kosa kubwa ambalo wapiganaji hao wa ufisadi walilifanya ni kukubali kuachia hoja ya Richmond ifungwe Bungeni wakati tayari walikuwa wamejiweka katika nafasi nzuri.
Aidha, woga wao wa kuhofia kufukuzwa kwenye chama umewaponza wengi, lakini kama wangethubutu pengine wangeondoka kama mashujaa na ushindi juu na leo hii wangesimama mbele ya Watanzania na kujipambanua kwamba ni wapinga ufisadi, hivyo wangeungwa mkono na wapiga kura wengi.
Wapambanaji hawa wanashindwa pia kuelewa kwamba, wamejimaliza wenyewe kwa kuwa wanafiki, kwa sababu kipindi chote cha kuanzia Septemba 2007 hadi leo hii wameonyesha juhudi tu za kufichua ufisadi lakini hawajaonyesha njia za kupambana ama kukomesha ufisadi huo.
Inaelezwa pia kwamba, kitendo cha ‘kumtoa kafara’ mpambanaji mwenzao, Fred Mpendazoe Tungu, waliyemtanguliza kwenye Chama cha Jamii kinachodaiwa kuanzishwa kwa ushirikisho wa baadhi ya wapambanaji hao, nacho kimewapunguzia nguvu kwa wananchi kwani wameshindwa ‘kumfuata’ huko alikokwenda.
Wananchi wengi wanasema wapambanaji hao waliitumia hoja ya Richmond kujipatia umaarufu badala ya ukombozi wa Taifa.
Naamini wanacholilia ni mbinu chafu zinazofanywa dhidi yao za kuwanyima wananchi fursa ya kuwachagua tena, mbinu ambazo wakati mwingine kwa maoni yao zinapakana na vitendo vya uhalifu na ndio maana wanataka vyombo vya sheria vifuatilie.
Lakini hapa pia wanashindwa kutambua kwamba, mbinu walizoingilia wao madarakani ndizo hizo hizo ambazo zinatumiwa na wale wanaotangaza dhamira ya kugombea majimbo hayo. Sijajua kwa nini hawa wabunge walio madarakani wanalia ovyo utadhani majimbo ni 'mali yao'. Tatizo wanataka kuziba njia ambazo wao walipitia, ili wanaokuja wasipite hizo, wakati njia hizo ndizo za mkato za kuelekea kwenye unono.
Kama kuna mbunge yeyote anayeweza kujigamba kuwa hakutumia mbinu chafu kuwalainisha wapiga kura na aseme sasa. Kila mbunge ama katoa chakula, au katoa chochote japo hata "kitochi" ili akumbukwe kwenye kura. Bila shaka wanaowania nao wanatumia mbinu hizi ili waonekane kwa mpiga kura. Takrima ilishapigwa marufu kisheria lakini bado kuna vijitarima vinaendelea pamoja na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kutoa onyo.
CCM inajinasibu kwamba ina uhakika wa kutwaa majimbo mengi mwaka huu, lakini zipo taarifa kwamba kuna wabunge zaidi ya 100, wakiwemo nusu ya mawaziri wa sasa, hawauziki na CCM inapaswa kuwa makini kutoyarudisha majina ya wabunge hao (wenyewe wanawajua) ili kukiepusha chama na kushindwa katika majimbo yao. Kimsingi CCM inapaswa kusimamisha wagombea wanaokubalika kama kweli inataka kushinda.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM taifa (NEC), Bw. Salum Msabah, alipata kukaririwa Februari 26, 2008 mkoani Mara wakati akizungumza na viongozi wa chama hicho, kwenye mikutano ya ndani, katika kata ya Kibara na Nansimo wilayani Bunda, kwamba tayari makao makuu ya chama hicho wamekwishabaini wabunge hao kuwa wakirudi utakuwa mzigo kwa chama hicho na iwapo watagombea tena katika uchaguzi wa mwaka 2010 majina yao hayatapendekezwa na uongozi wa juu wa chama hicho. Kwa muda mrefu baadhi ya wabunge hao wamekwisha kuwa kero kwa wananchi kwa kuwa wakichaguliwa hawarudi tena kwenye majimbo yao na badala yake wanakuwa watu wa mijini tu.
Utafiti uliofanywa na asasi isiyo ya kiserikali ya Nyota, umeonyesha kwamba zaidi ya nusu ya mawaziri waliotajwa kuwa makamanda katika Serikali ya Awamu ya Nne wanaweza kupoteza nafasi zao za ubunge na hali ni tete katika majimbo ya mawaziri hao kutokana na wananchi wengi wa majimbo hayo kukosa imani nao.
Taarifa ya awali iliyotolewa na Mratibu wa asasi hiyo, Vincent Kornald Mkisi, ilisema kuwa mazingira ya mawaziri na manaibu hao kupoteza nafasi zao yalianza kuonekana tangu Januari 2010 na mawaziri walio katika hali mbaya kurudi bungeni ni pamoja na Profesa Peter Msolla ambaye anakabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Kilolo, Venance Mwamoto ‘Motto’.
Duru za kisiasa zinasema kuwa Profesa Msolla alitarajia kudra za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuligawa Jimbo la Kilolo na kuwa mawili, hivyo alijipanga kuwania ubunge katika eneo la Ilula ambako anakubalika zaidi kuliko maeneo mengine.
Waziri mwingine anayetajwa kuwa katika kaa la moto kwa mujibu wa utafiti huo, ni Profesa Jumanne Maghembe, anayekabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa mwanasheria wa kujitegemea, Joseph Tadayo. Inaelezwa kuwa baada ya Tadayo kuweka bayana nia ya kuwania ubunge katika Jimbo la Mwanga, waziri huyo alianza mkakati wa kutumia nguvu kulazimisha kukutana na wazee kwa nia ya kuwaweka sawa na kujihakikishia kuilinda nafasi yake ya ubunge.
Hata hivyo, Profesa Maghembe anapaswa kujilaumu mwenyewe kutokana na kile ambacho wananchi wa Mwanga wamekuwa wakikitaja kuwa ni ubabe na kujiona ana haki ya kifalme ya kuliwakilisha jimbo hilo. Watafiti wanasema ameshindwa kuwaunganisha wananchi wa Mwanga, na kwamba hata waziri mkuu mstaafu ambaye pia alikuwa mbunge wa jimbo hilo, Cleopa David Msuya, hakubaliani naye.
Nyota imeonyesha kuwa pamoja na kuwa sura za vijana katika Baraza la Mawaziri ilionekana kuwa nuru mpya kwa wananchi na kuwafanya kuwa na imani na Serikali ya Rais Jakaya Kikwete, mawaziri wake wawili vijana, William Ngeleja wa Nishati na Madini na Dk. Lawrence Masha wa Mambo ya Ndani wako juu ya kaa la moto.
Ngeleja anakabiliwa na mchumi mwandamizi na mwanamageuzi wa kilimo anayeendana na falsafa mpya ya ‘Kilimo Kwanza’, Francisco Kimasa Shejamabu, ambaye pia ni meneja na mmiliki mwandamizi wa Kampuni ya Tanwat ya jijini Mwanza.
Habari zinasema kuwa Ngeleja alikuwa akiandaa mkakati wa kutaka matawi na kata za CCM katika Jimbo la Sengerema kutoa tamko la kumtangaza kuwa mgombee pekee ili aweze kupitishwa bila kupingwa. Hata hivyo, inaelezwa kuwa mpango wake huo umekwama kutokana na kuwapo kwa kundi kubwa la wanachama wa CCM walioamua kupingana na dhana hiyo na kutaka kuwapo demokrasia ndani ya chama chao.
Mwingine anayekabiliwa na hali mbaya ni Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo, Kapteni George Huruma Mkuchika (Newala), Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Diodoros Kamara (Nkenge), Waziri wa Sheria na Katiba, Mathiasi Chikawe (Nachingwea), Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkullo (Kilosa Kati), Waziri wa Kilimo na Chakula, Stephen Wassira (Bunda) na Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Mary Nagu (Hanang).
CCM inapaswa kusikiliza kilio cha wananchi kuhusu suala la wabunge kung’ang’ania madaraka kwa ajili tu ya kujipatia mishahara mikubwa, posho na mafao lukuki bila kutambua kwamba wanapaswa kuwatumikia wananchi. Hili limekuwa siyo siri tena, hasa katika kipindi hiki ambacho wananchi wanaelewa hata mambo yanayoendelea sirini. Wabunge wazee na wale walioshindwa kutekeleza majukumu yao ya uwakilishi wa wananchi wanatakiwa wasipate ridhaa ya wananchi tena hata kama watapitishwa na vyama vyao, huo ndio uwe msimamo wa Watanzania kama kweli wanataka kujiletea maendeleo.

SOURCE: DIRA YA MTANZANIA.

No comments:

JUST ANOTHER THOUGHT

JUST ANOTHER THOUGHT

A person asked God, “What surprises you most about mankind?”

And God answered,
“That they loose their Health to make money and they loose their money to restore their Health.

That by thinking anxiously about the future, they forget the present, such that they live neither for the present nor the future.

That they live as if they will never die and they die as if they had never lived.….”

BECAUSE I'M A MAN...

Because I’m a man, when one of our appliances stops working I will insist on taking it apart, despite evidence that this will just cost me twice as much once the repair person gets here and has to put it back together.

Because I’m a man, I don’t think we’re all that lost, and no, I don’t think we should stop and ask someone. Why would you listen to a complete stranger I mean, how the hell could he know where we’re going?

Because I’m a man, there is no need to ask me what I’m thinking about. The answer is always either sex or football, though I have to make up something else when you ask, so don’t.

Because I’m a man, I do not want to visit your mother, come visit us, or talk to her when she calls, or think about her any more than I have to. Whatever you got her for mother’s day is okay, I don’t need to see it. And don’t forget to pick up something for my mommy, too!

Because I’m a man, I am capable of announcing, “one more beer and I really have to go”, and mean it every single time I say it, even when it gets to the point that the one bar closes and my buddies and I have to go hunt down another. I will find it increasingly hilarious to have my pals call you to tell you I’ll be home soon, and no, I don’t understand why you threw all my clothes into the front yard. Like, what’s the connection?

Because I’m a man, you don’t have to ask me if I liked the movie. Chances are, if you’re crying at the end of it, I didn’t.

Because I’m a man, yes, I have to turn up the radio when Bruce Springsteen or The Doors comes on, and then, yes, I have to tell you every single time about how Bruce had his picture on the cover of Time and Newsweek the same day, or how Jim Morrison is buried in Paris and everyone visits his grave. Please do not behave as if you do not find this fascinating.

Because I’m a man, I think what you’re wearing is fine. I thought what you were wearing five minutes ago was fine, too. Either pair of shoes is fine. With the belt or without it looks fine. Your hair is fine. You look fine. Can we just go now?

Because I’m a man and this is, after all, the 90’s, I will share equally in the housework. You just do the laundry, the cooking, the gardening, the cleaning, and the dishes. I’ll do the rest.

A SIMPLE GUIDE TO LIFE

1. Follow your dream! Unless it’s the one where you’re at work in your underwear during a fire drill.

2. Always take time to stop and smell the roses and sooner or later, you’ll inhale a bee.

3. Do not walk behind me, for I may not lead. Do not walk ahead of me, for I may not follow. Do not walk beside me, either. Just leave me alone.

4. If you don’t like my driving, don’t call anyone. Just take another road. That’s why the highway department made so many of them.

5. If a motorist cuts you off, just turn the other cheek. Nothing gets the message across like a good mooning.

6. When I’m feeling down, I like to whistle. It makes the neighbor’s dog run to the end of his chain and gag himself.

7. It’s always darkest before dawn. So if you’re going to steal the neighbor’s newspaper, that’s the time to do it.

8. A handy telephone tip: Keep a small chalkboard near the phone. That way, when a salesman calls, you can hold the receiver up to it and run your fingernails across it until he hangs up.

9. Each day I try to enjoy something from each of the four groups: the bonbon group, that salty-snack group, the caffeine group and the “What ever-it-is-the-tinfoil-in-the-back-of-the-fridge”.

10. Into every life some rain must fall. Unusually when your car windows are down.

11. Just remember: You gotta break some eggs to make a real mess on the neighbor’s car!

12. When you find yourself getting irritated with someone, try to remember that all men are brothers and just give them a noogie.

13. This morning I woke up to the unmistakable scent of pigs in a blanket. That’s the price you pay for letting the relatives stay over.

14. It’s a small world. So you gotta use your elbows a lot.

15. Keep your nose to the grindstone and your shoulder to the wheel. It’s a lot cheaper than plastic surgery.

16. This land is your land. This land is my land. So stay in your land.

17. Love is like a roller coaster: When it’s good you don’t want to get off, and when it isn’t, you can’t wait to throw up.

DEDICATION TO YOUNG PEOPLE

Youth is a time of hope. Also of uncertainty. But for a person who is young and healthy, uncertainty just means a challenge. It is important to be positive. First of all about yourself. But also about your family and your people. As a unique person and each human being are unique, you have enormous potential. Because you have so much potential, people may sometimes feel negatively challenged by that potential and try to undermine it.

You have to fight for your right to make your place in society. To do that you have to use all the chances given you now to be a positive element in whatever situation you find yourself in, in future. So, it may be necessary to be a ‘rebel in reverse’ as it were. That takes real courage, to set your goal and stick to it. You choose your crowd. You exercise your right to choose.
Don’t lose your freedom for the sake of anyone. Real freedom, freedom to choose the right thing, the best for you.

Always bear a few things in mind while exercising your right to choose.

* Never take a decision when you are in a fit of anger or depression.
* Never take a decision when you are emotionally high.
* Why should fads or the decision of the group tie you down?
* What are you?
* What do you want tomorrow to be for you?

No matter how strong the group decision may be, you must think and make your decision. Many times it is necessary to consult before taking a decision. Go to someone whose life you admire, not necessarily the person you like most, but the person who is whole, who is one person, wherever she or he is and whatever she or he does.

* Remember that there is always tomorrow, and tomorrow is hope. Very few things are ‘written in stone’. Most of the mistakes we make can be rectified. They can be corrected. Problems have a solution, and each new day is a new start, a new chance, a New Hope. Indeed the youth are our hope you are our future.

Also remember that your parents love you unconditionally, you have their support and want the best in life for you ¨

COSTA VICTOR NAMPOKA

Mguu ulivyokatisha ndoto za kucheza soka Ulaya

DANIEL MBEGA
Dar es Salaam

NI majira ya saa 5.20 hivi asubuhi, niko hapa Ukonga-Banana nikiwania kupanda daladala la kwenda kwenye kitongoji cha Kitunda-Kibeberu, moja ya vitongoji vinavyokua kwa kasi hapa jijini Dar es Salaam.
Sijui ni umbali gani kutoka hapa, hivyo namuuliza dereva ambaye nimeketi naye pembeni yake. Ananiambia ni mwendo kama wa dakika 15 tu hivi. Nashusha pumzi kwa kujua kwamba kumbe si mbali sana kama nilivyofikiria.
Nawasili kwenye kitongoji cha Kibeberu, ambako ndiko magari yanakogeuzia, na bila kupoteza muda nampigia simu mwenyeji wangu kwamba tayari nimeshafika. Namhurumia huko aliko kama ataamua kuja kunipokea, lakini nafarijika anaponiambia kwamba nimuulize mtu yeyote hapo kituoni atanileta.
Watoto wawili wanajitolea kunipeleka nyumbani kwa mwenyeji wangu, ambaye namkuta akiwa kajilaza kwenye kochi akizungumza na rafiki zake wawili waliomtembelea. Anapenda kuketi vizuri, lakini hali haimruhusu.
“Poleni jamani kwa safari ndefu!” ndivyo anavyoanza kusema huyu mwenyeji wangu, ambaye si mwingine zaidi ya mlinzi mahiri wa timu ya soka ya Taifa, Taifa Stars, pamoja na klabu ya Simba, Costa Victor Nampoka ‘Nyumba’. Anajaribu kuuweka vyema mguu wake wa kulia ambao bado umefungwa bandeji gumu (POP) baada ya kuvunjia mazoezini takribani mwezi mmoja na nusu uliopita.
“Hakuna shaka, Dar es Salaam ni moja na hakuna sehemu unayoweza kusema ni mbali,” namjibu kumpa matumaini.
“Hapana! Pamoja na ukweli kwamba mkoa kazini, lakini naamini uamua kufunga safari mpaka kuja kuniona ni jambo kubwa sana. Mngeweza hata kuniuliza maendeleo yangu kwa njia ya simu. Sina budi kushukuru kwa kuja kunijulia hali,” anasema.
Mara anaingia dada mmoja mweupe hivi ambaye anaketi pamoja na Costa kwenye kochi moja. Costa mwenyewe anamtambulisha kwamba ndiye mkewe, Dina, ambaye wamebahatika kuzaa naye watoto wawili; Victor Costa mwenye miaka miwili na Rio Costa mwenye mwaka 1.5. Anatukaribisha.
Anapoondoka namwambia ni jambo la kawaida kuwatembelea wagonjwa, na katika suala lake yeye ni mmoja wa watu waliotoa mchango mkubwa katika timu ya taifa ya soka ambayo sasa iko katika nafasi nzuri ya kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika mwakani ikiwa tu itashinda mechi yake ya mwisho.
“Nashukuru kusikia hivyo, lakini sura zinazokuja hapa daima ni zile nilizozizowea, yaani marafiki zangu na wachezaji wenzangu wa klabu ya Simba, labda na viongozi wa Simba,” anasema kwa huzuni.
“Una maana kwamba viongozi wa timu ya taifa na hata TFF huwa hawakutembelei?” nauliza.
Anasema tangu alipoumia siku tatu kabla ya Taifa Stars kupambana na Zambia katika mechi ya kirafiki na kupelekwa Muhimbili na daktari wa timu Shecky Mngazija, hajatembelewa wala kujuliwa hali hata kwa simu na kiongozi yeyote yule wa chombo hicho cha juu cha soka nchini.
Anaongeza kwamba, ni wachezaji wenzake wa Simba ndio baadhi yao huwa wanawasiliana naye pamoja na viongozi na marafiki wa klabu ambao wameonekana kumjali vya kutosha kiasi cha kutuma gari kila siku katika mechi zote ambazo Simba ilicheza kwenye hatua ya Sita Bora ya Ligi ya Mpito hadi fainali.
“Kwa kweli viongozi wa klabu yangu wananijali sana na sina budi kuwashukuru,” anasema. Kama vile amekumbuka kitu, anasema anamshukuru pia mtu mmoja wa Benki ya NMB anayeitwa Kajura (Imani Kajura ambaye ni Meneja Masoko).
“Huyu jamaa baada ya kutoa zawadi za shilingi 500,000 kwa kila mchezaji kutokana na timu ya Taifa kushinda kule Burkina Faso, alinipigia simu kuniambia nilitakiwa kwenda kusaini fomu za akaunti. Nikamwambia sina hata pesa ya nauli na kwa jinsi ninavyoumwa nisingeweza kupanda daladala, lakini akaniambia nichukue teksi nay eye angelipa. Namshukuru sana,” anasema.
Hata hivyo, amewaasa wachezaji wengine; wa klabu na hata timu ya taifa, kwamba pindi watakapoumia na kushindwa kujuliwa hali na viongozi wao wasife moyo bali hiyo iwe changamoto kwao kufanya vizuri watakaporejea uwanjani.
“Binafsi sina kinyongo na yeyote. Naomba Mungu nipone nirejee uwanjani, ikibidi niliwakilishe taifa langu, kwa sababu natambua kwamba timu ya Taifa ni ya Watanzania wote wala si ya mtu mmoja. Naamini Watanzania milioni kadhaa wako pamoja na mimi na hata walipojua kwamba nimeumia walinitumia meseji za pole zaidi ya 3,000, hata sijui walikoipata namba yangu,” anasema.

Kuvunjika mguu
Costa anasema kwamba walikuwa kwenye mazoezi kama kawaida kwenye uwanja wa Karume, akauzuia mpira bila kumkwatua ama kukwatuliwa, kisha akaserereka.
“Ghafla nikasikia maumivu makali sana, ikabidi wajaribu kuniganga pale, lakini yalipozidi wakanikimbiza Muhimbili. Huko nikaambiwa kwamba nimevunjika mfupa mdogo wa mguu wa kulia. Sikuwa na jinsi, wakanifunga hogo (bandeji gumu – POP) na kusema kwamba nirudi baada ya wiki sita,” anasema kwa majonzi.
Anasema kwamba, baada ya kutolewa kwa bandeji hilo ndipo atakapojua kama atakuwa nje ya uwanja kwa muda gani, kwani mpaka sasa hajaanza hata kuukanyangia mguu huo.
Akasema kuvunjika mguu kumemnyima nafasi ya kuliwakilisha taifa, na zaidi kumechelewesha kutimia kwa ndoto zake kwani pengine hivi sasa angeweza kuwa Afrika Kusini kujaribu kucheza soka ya kulipwa akiwa njiani kwenda cheza Ulaya.
“Kuna wakala mmoja ambaye kwa muda mrefu sasa amekuwa akinufuatilia, yuko Afrika Kusini, na alikwenda Burkina Faso kunitazama, lakini mimi sikuwepo. Ilikuwa niende Afrika Kusini kufanya majaribio na naamini ningewea kufanikiwa,” anasema mchezaji huyo.
Anasema kwamba, alikuwa na matumaini ya kufuzu kwa sababu soka ya Afrika Kusini haina tofauti na ya huku, tena hakuwa mgeni baada ya kucheza kwa muda nchini humo miaka mitatu iliyopita.
“Wanachotuzidi kule ni promosheni, televisheni zinajitahidi sana kuonyesha mpira hata wa daraja la tatu, na hiyo inamsaidia mchezaji kutazama na kuona wapi alipokosea ili kujirekebisha, ama afanye nini kuongeza jitihada,” anasema.
Anaongeza kwamba alishindwa kuendelea kucheza huko kwa sababu klabu aliyokuwa akiichezea wakati ule ya Marlasburg (Tembas) iliyokuwa daraja la kwanza mwaka 2005 ikiwa chini ya kocha wa zamani wa Simba Trott Moloto, iliinunua klabu moja iliyokuwa ligi kuu. Ikabidi wachezaji wa timu hizo wachekechwe, na majungu ndipo yakaibuka ambapo Moloto, ambaye ndiye aliyemfanyia mpango wa kwenda huko, akamgeuka. Ikabidi afungashe virago kurejea.
Hata hivyo, anasema kwamba ndoto zake bado hazijafutika, kwani anaamini anaweza kucheza Ulaya bila matatizo yoyote, na zaidi anasema angependa siku moja avae ‘uzi’ wa Manchester United akicheza pembeni ya Rio Ferdnand ambaye uchezaji wake unamvutia kiasi cha kumwitia mwanawe mdogo jina hilo kutokana na kumhusudu.
Akizungumzia nafasi ya Taifa Stars kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika mwakani, Costa (25) ambaye ni mtoto wa nne katika familia ya watoto watano wa mzee Victor Nampoka – wawili wanawake na watatu wanaume, anasema kwamba nafasi ipo, lakini mechi ya mwisho dhidi ya Msumbiji ni ngumu sana.
“Ile mechi ni kama fainali na inabidi maandalizi ya nguvu yafanyike pengine kuliko mechi zote zilizotangulia. Msumbiji ni wazuri sana kuliko hata Burkina Faso, na ina nafasi ya kufuzu ikiwa itashinda na Senegal wakafungwa, hivyo Watanzania tusibweteke bali tujiandae vizuri,” anasema huku akisikitika kwamba anaweza kuikosa mechi hiyo pia ikiwa ataambiwa apumzike.
Akizungumzia kuhusu maendeleo ya soka, mlinzi huyo anasema kwamba hakuna kitakachoinua zaidi ya soka la vijana, na kuongeza kwamba mashindano ya Copa Coca Cola yawe chachu wa klabu na wadau mbalimbali kuanza kuibua vipaji.
“Kule Brazil tulikokwenda kuna taasisi ya soka ya watoto wadogo. Watoto wanatoka nchi mbalimbali kwenda kufundishwa mpira, na wazazi wao wanalipia wastani wa dola 1,500 kwa mwezi ili watoto wao wajue mpira. Tusione wenzetu wamepiga hatua tukadhani kwamba ni miujiza, wamewekeza.
“Watanzania wanapaswa kuunga mkono juhudi za maendeleo ya soka ya vijana, kuanzia kwa wazazi, ambao wanapaswa kuwapa ‘sapoti’ watoto wao ikiwa ni pamoja na kuwapatia vifaa vya michezo na nauli ya kwenda mazoezini,” anaongeza.
Costa aliyemaliza elimu ya msingi mwaka 1994 Kinondoni Hananasif, jijini Dar es Salaam na kuungana na maelfu ya watoto ambao hawakufanikiwa kuchaguliwa kujiunga na sekondari, amewashauri wachezaji kuachana na anasa na kwamba wawe na malengo kama kweli wanataka kupiga hatua katika mchezo huo.
“Sijafanikiwa sana, lakini niseme ukweli kwamba nimejiepusha na mambo mengi. Sivuti sigara wala bangi, halafu niliacha kitambo kunywa pombe, tena basi nilikuwa nikinywa bia mbili ama tatu tu, lakini sasa sitaki kabisa nahitaji kukazana kwenye mpira ambao pekee ndio mwokozi wangu katika maisha,” anamalizia.

Wasifu:
Jina: Costa Victor Nampoka
Kuzaliwa: Oktoba 11, 1982, Dar es Salaam.
Umri: 25

Klabu za awali:
Five Star Kinondoni, Mkunguni FC Ilala, Eleven FC Buguruni, Saddam FC na International FC za Kinondoni.
Taifa Jang’ombe – Zanzibar (1998 – 1999)
Forodha Zanzibar (2000 – 2001)
Mtibwa Sugar (2002)
Simba (2003 – 2004)
Marlsburg – Afrika Kusini (2005)
Simba (2006 – mpaka sasa).